Pekua/search

Monday, September 28, 2009

UPOLE: WOULD YOU CALL THIS CHILD LABOUR? I DO NOT!!

http://www.facebook.com/home.php?ref=home#/profile.php?id=1290373856&ref=nf

CAN'T THESE BE LESSONS FROM THE RURAL SIDE OF TANZANIA??

Mr. Kiswigu, a resident of Mbambo village in Rungwe district, Mbeya- Tanzania is reputed for his close involvement in nursing his child. what a relief to his wife!!
Mr. Kiswigu who is also handcapped, is full of abilities and a rich heart
Steven, Abas, and Frank, kids of less than ten years of age, working on their grandmother's farm.

Rural side of life is rich, very rich if u like in terms of experiences and all. My tour, recently at Mbambo village, Rungwe district, Mbeya- Tanzania has the following modest learnings. Judge for yourself on each photo as it speaks a thousand words.

Sunday, September 27, 2009

WOULD YOU CALL THIS CHILD LABOUR? I DO NOT!!

WOULD YOU CALL THIS CHILD LABOUR? I DO NOT!
click to watch the clip



The three kids, Steven, Abas and Frank 'volunteering?' on their grandmother's maize field at Mbambo village, Rungwe district, Mbeya- Tanzania. 'Interview in kinyakyusa and Kiswahili asking for names and the owner of the farm'.
Mwonyeshe njia njema mtoto naye hataiacha!!

Thursday, September 24, 2009

How Chenge played major role in corrupt radar negotiations

How Chenge played major role in corrupt radar negotiations
Source: Tanzanian Corruption tracker

The Bariadi West Member of Parliament, (CCM), Mr Andrew John Chenge who was Attorney General between 1995 and 2006 is alleged to have played a major role in the corrupt negotiations for the purchase of the controversial radar system for installation at the Dar es Salaam’s Mwalimu Julius Nyerere International Airport.

According to investigations carried out by the British Serious Fraud Office, SFO, on what has now come to be known as the radar scandal, Mr Chenge is not only alleged to have played a major role in the negotiations for the purchase of the radar, but also helped in facilitating its conclusion. The SFO says in part: “Chenge became directly involved with numerous aspects of the contract negotiations, notably the financing of the purchase”.To read the whole story click here

TUJADILI MIHTASARI MIPYA YA MAFUNZO YA UALIMU 2009

Ndg wadau

Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi wiki iliyopita ilitoa miongozo mipya [Sylabus] kwa ajili ya kufundishia katika vyuo vya Ualimu kwa ngazi zote za cheti na stashahada.Kupata miongozo hiyo Bonyeza HAPA

Na John Malata

Chanzo: Wanazuoni yahoo groups

Adam alichangia ifuatavyo:

Amani kwako John na wanazuoni.

Shukrani kwa kutupa ujumbe huu muhimu. hata hivyo nanalo dukuduku, ninaomba wanazuoni weledi mnisaidie, mkiweza.

Hii mihtasari iliyotolewa inahusiana vipi na Sera mpya ya Elimu na Mafunzo 2009, ambayo ndiyo kwanza 'inaandaliwa' ?

Je kimantiki haikupaswa sera mpya itangulie kuwepo ndipo mihtasari ambayo kimsingi ni miongozo inayoelekeza utakelezaji ambao utawezesha kufikiwa kwa matamko ya sera kisha kufikiwa kwa malengo ya sera husika na hatimaye malengo makuu ya taifa, Dira ya Maendeleo ya taifa?

Kwa ufahamu wangu mdogo Sera inatoa mwongozo wa jumla na kisha mipango mbali mbali na mihtasari kama hiyo ndiyo inaelekeza kinagaubaga (kitaalamu) namna ya kutekeleza. Baada ya kuyazingatia maelekezo yaliyomo kwenye sera ndipo miongozo mbali mbali, ikiwemo mihtasari inapaswa kuandaliwa. Sasa kama hivyo ndivyo kwanini mihtasari mipya ya mafunzo ya ualimu (ambayo kwa kiasi kikubwa ni muhimili muhimu wa kutekeleza sera) inatolewa mapema? tutakuwa na uhakika gani kwamba mihtasari hiyo haijafuata malekezo ya sera ya zamani? na kama sivyo, je ndiyo kusema sera mpya inayojadiliwa sasa tayari imepitiswa na kinachofanyika hivi sasa (kupata maoni ya wadau) ni usanii tu?

Je hauwezi huu kuwa ufisadi, tena mbaya kuliko aina nyingine za ufisadi? Sera haijatoka, mihtsari inatolewa, kwa haraka gani? Kwa faida ya nani? nisaidie jamani!!! Huenda hili sio kosa dogo. Kama walimu wakiandaliwa tofauti na maelekezo ya sera, je si hatari iliyoje?

Nawasilisha

Wednesday, September 23, 2009

COULD THIS QUOTE INSPIRE WOMEN?


“If the first woman God ever made was strong enough to turn the world upside down all alone, these women (of today) together ought to be able to turn it back, and get it right side up again!”

Sojourner Truth (1851)

Tuesday, September 22, 2009

KUJIFUNZA KWA SALMA KIKWETE KUHUSU KISWAHILI


Matumizi ya Kiswahili: Tuna la kujifunza kwa Mama Salma Kikwete.
Na Lingson Adam

Wadau makala haya yalichapishwa kwenye gazeti la Sauti Huru mwezi Mei mwaka huu (2009) kuendeleza mjadala wa MATUMIZI na Fahari yetu kwa Kiswahili nimeona vema kuuweka hapa kama sehemu ya kuendeleza mjadala.

Pichani Mama Salma akikabidhi kabrasha kuhusu mipango ya WAMA kwa naibu mkurugenzi mtendaji wa UNICEF mama Hilde Johnson ambaye anakichapa Kiswahili barabara.Picha kutoka blogu ya Michuzi

Tangu alipoingia madarakani, Rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, mkewe, first Lady Salma Kikwete pichani (kutoka blogu ya Michuzi)
kushoto, amekuwa mstari wa mbele katika harakati mbalimbali. Harakati zake hizo zimejipambanua zaidi katika kuanzisha na kuendesha
kwa ufanisi shirika la Wanawake na Maendeleo – WAMA, ambalo yeye ni mwenyekiti.

Katika harakati hizo mama Salma, amekuwa akikaribisha na kupokea wingi wa wageni mbali mbali kutoka mataifa ya karibu na mbali.

Mara nyingi, kama si zote, mama Salma amekuwa(alikuwa) akitumia Kiswahili katika hotuba zake kwa wageni wake. Ni katika suala hili ambapo nadhani mama Salma anastahili pongezi, kuungwa mkono na kujifunza kutoka kwake.

si ajabu kwamba mwanzoni wengi wetu tulidhani ni kutokana na yeye kutokuwa bingwa katika lugha ya Kiingereza, lakini nadhani mpaka sasa tumejihakikishia kwamba tulichemka. Mama huyu Mwalimu kitaaluma na kitaalamu, anakijua Kiingereza vizuri kabisa, walau sawa tu na viongozi wetu wa kiume na wakike waliowengi.

Mrengo aliouchukua mama Salma nadhani ni wa maksudi kabisa. Aliamua toka mwanzo kabisa kujipambanua kuwa ni Mtanzania anayejivunia Kiswahili.

Mama Salma amekuwa mstari wa mbele kueleza bayana umuhimu wa Kiswahili. Akiwa safarini nchini Marekani na Uingereza hivi karibuni, alitoa changamoto kwa watanzania waishio katika nchi hizo kuongea Kiswahili fasaha na kujivunia lugha hiyo adhimu. Mama Salma alieleza bayana kwamba Kiswahili ni raslimali muhimu ya watanzania

Mama Salma amekuwa mara kwa mara akiwashaajisha watanzania kuwa ni muhimu waenzi utamaduni wao, na kwa kutumia Kiswahili watakuwa wametekeleza suala hilo kwa namna ambayo ni ya msingi sana pengine kuliko njia nyinginezo za kujipambanua kiutamaduni.

Katika suala hili mama Salma amejitoa na ametutoa kimasomaso na kwa hakika amekuwa mfano hata kwa mumewe, Rais wetu Jakaya Kikwete ambaye naweza kusema anakionea aibu Kiswahili.

Rais kupoteza fursa

Rais Kikwete mara nyingi amekwama kutumia fursa nyeti za kuitambulisha Tanzania kuwa mama au baba wa Kiswahili. Mathalani alipigwa mwereka na Rais wa Kenya Mwai Kibaki na Waziri Mkuu wake Raira Odinga huko Nairobi, mwanzoni mwa mwaka jana katika hadhara muhimu kabisa ya kimataifa. Baada ya kufanikiwa kuwaweka pamoja ndugu hao wa Kenya, Rais Kikwete kwa nafasi yake akiwa kiongozi mkuu wa Umoja wa Afrika wakati huo, alitoa hotuba yake kwa Kiingereza.

Kama Rais wa Tanzania anatoa hotuba kwa Kiingereza katika eneo la Afrika Mashariki, nani abebe bendera ya Kiswahili duniani? Tofauti na kiongozi huyo wa Umoja wa Afrika, 'faraja' ikaja pale Odinga na Kibaki walipohutubia kwa Kiswahili. na ndiyo maana ninasema walimpiga mwereka Kikwete wetu hawa Wakenya! na walitupiga mwereka mbaya sana watanzania wote hawa ndugu zetu!

Ni rahisi kuuchukulia kirahisi mfano huu, lakini uzito wa jambo linalofanywa na kiongozi wa jamii au nchi fulani hauwezi kupuuzwa. Afanyacho kiongozi wa watu, asemacho kiongozi wa watu kinabeba, kwa asilimia kubwa, nadhani kubwa kabisa, taswira ya jamii au taifa analoliongoza.

kwa hili, mtoto wa taifa la mbali aliyekuwa akisikiliza hotuba hizo na angetokea kuuliza wazazi wake ni lugha gani Kibaki na Odinga walikuwa wakiiongea na akaambiwa ni Kiswahili, basi atajua Kiswahili ni lugha ya Kenya. Haina ubaya wakenya kuongea Kiswahili, lakini utambulisho wetu unapotea. rais wetu alipoteza furasa. na amepoteza nyingi za aina hiyo. viongozi wetu wengi mawaziri kwa wanadiplomasia wengi wengine, wamepoteza fursa hizo

Kiswahili kama fursa na raslimali inayopotezwa

Tunayorekodi watanzaia, rekodi mbaya na chungu kuikubali. Tunaelezwa na wenzetu wa karibu na waliotoka mbali, naam hata sisi wenyewe tunajua na kufahamu kwamba tumebobea katika kupoteza ama kutotumia ipasavyo fursa nyeti za kutuendeleza. Moja ikiwa ni mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kuliko yote barani Afrika.

Imeelezwa kwa miaka mingi kuwa pamoja na mwenyezi Mungu kutujaalia utajiri wa raslimali za kipekee Afrika na duniani, watanzania hatujaweza kuzitumia vema fursa na raslimali hizo kutusaidia kuishi vema zaidi. Mlima Kilimanjaro umekuwa kwenye rekodi ya juu kuwa umetumika kwa tija zaidi na jirani zetu wa Kenya kuvutia utalii. Ahueni imekuja walau miaka ya karibuni tulipoanza kuutangaza japo ‘kizembe zembe fulani’.

Kama kuongeza na chumvi kwenye jeraha la mtu, tumeelezwa na kuchekwa kuwa hatujatukuka duniani kuwa wauzaji wanaoongoza wa madini ya TANZANITE yanayopatrikana Tanzania pekee!

Kiswahili kama lugha ambayo licha ya historia yake kuhusisha upwa wa Afrika mashariki katika mapana na marefu yake, bado ni Tanzania ambayo ilijipambanua kihistoria kuwa mwenye kuitumia lugha hiyo kitaifa tangu wakati wa harakati za kupigania uhuru na baada ya uhuru.

Hata hivyo, hatujaitumia fursa ya kuwa ‘wamiliki’ wa lugha hii kututajirisha wakati ndiyo lugha pekee yenye uwezekano wa kuwa lugha ya mawasiliano kwa nchi zote za Afrika ya mashari kati na kusini. Hakuna lugha nyingine yenye fursa kama ya Kiswahili kwenye eneo hili. Lugha hii ingeweza kupanua soko letu la kuajirika ndani na nje ya mipaka yetu. Utashangaa leo hii, watanzania tukinyong’onyezwa nasi kunyon’gonyea kwa madai ya kizandiki eti ‘watanzania hatuajiriki sana kimataifa zaidi ya wakenya kwa vile hatujui Kiingereza!!’

Tungetumia vema raslimali hii ‘Kiswahili’ tungezalisha wakalimani na wafasiri makumi kwa maelfu duniani, tungezalisha walimu wa lugha hii adhimu maelfu kwa malaki duniani, na hizo ni fursa ambazo tunazihitaji. Taarifa zinaonyesha walimu wengi wa Kiswahili duniani wanatoka nchini Kenya!

Hatari ya watanzania kutokutumia kwa faida Kiswahili inaelezwa na kufupishwa vizuri zaidi kwa hadithi ya UBINGWA MA NANYIGU na NYUKI KATIKA KUTENGENEZA ASALI aliyoniambia mwalimu wangu mzee Millinga.

Kwa mujibu wa hadithi ya mwalimu wangu huyo manyigu ndiyo yalikuwa mabingwa duniani katika kutengeza asali. Maprofesa wa kufundisha wadudu wengine kutengeneza asali walikuwa ni manyingu na wala hapakuwepo viumbe wa kufafanana nayo. Chuo kikuu cha kutengeneza asali kilikuwa na wahadhiri, manyigu, wahadhiri wabobezi na wazamivu wapatao 20. Hawa walitegemewa dunia nzima.

Sifa hizo zilizovuma na kuenea kama moto wa nyika zilifanya wanafunzi manyigu kujisikia wa daraja la juu ‘na kweli walikuwa’ kwa hiyo hawakufanya sana bidii kujifunza. Lakini nyuki, ambao hawakuwa na historia ya ubingwa huo, waliona fursa hiyo, wakawa nafanya bidii sana katika kujifunza, wakaujua ujuzi kwa jasho lao na kukosa usingizi!

Siku ya siku wahadhiri manyigu walikwenda kwenye tafrija, walisafiri mbali upande wa bahari wa nchi hiyo kwa ndege. Baada ya kufurahi na jioni walipokuwa wakirejea majumbani kwao, lisilotarajiwa likatokea, ndege ikapata hitilafu, ikaanguka na mabingwa wote wakateketea!!!

Hapakuwa na mabingwa manyigu tena, wanafunzi wa asili ya manyigu, hawakuwa makini kupakuwa ujuzi kutoka kwa ndugu zao, bali walishiriki sifa tu ya jamii yao. Huo ukawa mwanzo wa wanafunzi na wanagenzi wa nyuki kuchukua usukani maana walifanya bidii sana katika masomo yao waliyafahamu maarifa na kuujua ujuzi, na ndiyo hadi leo nyigu hayatengezezi masega ikajaa zaidi ya kiganja, lakini nyuki, nani asiyemjua?

Waasisi wa taifa waliiona fursa katika Kiswahili kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiuchumi, ulinzi na usalama. Wakajifunga kukikuza na kukiendeleza Kiswahili, wakatujengea sifa ya Kiswahili, tukaheshimika duniani. Lakini leo sisi Tanzania kama taifa tunafanya juhudi zipi za kuhakikisha tunazalisha wahitimu wengi wa Kiswahili? Vyuo vikuu vyetu vinatoa mabingwa wangapi wa Kiswahili jamani? Hawawezi kuwa wengi, maana hata watoto wetu hawawezi kurithi fahari ya lugha ya Kiswahili, kwa vile wanatuona tunavyoona fahari kwenye shule za michepuo ya Kiingereza, almaarufu ‘English medium’, wana wetu wanatuona tunavyofarijika wakiongea kizungu cha ‘yesi dadi’, yesi mami’ sijui fotokopi tugeza na kazalika’. Wanachorithi ni kuwa fursa iko katika kiingereza, lakini kweli? Kiswahili hakina fursa? Kiswahili kwa Tanzania kama taifa kinayo fursa kubwa sana, lakini ni ile iliyopotezwa, ni fursa iliyopuuzwa.


Mwelekeo wa mama Salma hauna budi kuigwa na kuungwa mkono na Viongozi wetu wa Kitanzania. Tunafahamu wanajua Kiingereza vizuri. Lakini wanalo jukumu la msingi kabisa la kukienzi Kiswahili. Wanalojukumu la Kukieneza na kukitangaza Kiswahili. Wanawajibika kukikona Kiswahili kama raslimali adhimu pengine hata zaidi ya Tanzanite, ambayo ikichimbwa inatoweka moja kwa moja.

Viongozi wetu katika ngazi zote, zaidi yetu sisi sote, wanalo jukumu la kukitumia Kiswahili kama fursa muhimu ya ajira. Viongozi wetu wanapaswa kutumia Kiswahili na hivyo kututafutia vijana wa kitanzania kazi za ukalimani, ufasiri na ualimu wa lugha hiyo huko ughaibuni. Wakiongea Kiswahili bila aibu haya yatawezekana sana.

Ni mara nyingi viongozi wetu wametumia Kiingereza pasipo hata na ulazima wa kufanya hivyo. Akiwepo mgeni mmoja tu kutoka nchi za mbali, basi viongozi wetu watamwaga Kiingereza, hata kama anakijua kidogo Kiswahili mgeni huyo.

Inafahamika wazi mathalan, kwamba Rais wetu akienda na ujumbe wake Uingereza, hawezi kuwafanya viongozi wa nchi hiyo wazungumze Kiswahili kkwa ajili yake. Vivyo hivyo akienda Uchina na Japani, watazungumza lugha zao viongozi wa nchini hizo, na ujumbe wa Tanzania utawasiliana na wenyeji wao kupitia Wakalimani na Wafasiri. Hiki ndicho alichokianzisha mama Salma. Anakimwaga Kiswahili mtoto wa Kitanzania.Wageni wake wanapata fursa ya kuuonja utamu wa lugha hii adhimu.

HONGERA MAMA SALMA. ENDELEA. KANYAGA TWENDE, HAKUNA KURUDI NYUMA. MJENGA NCHI NI MWANANCHI MWENYEWE.Inawezekana kabisa, isingekuwa utashi wa viongozi waasisi wa taifa hili, hata majeshi yetu yangekuwa yanatumia kiingereza katika kuamrisha gwaride.

Inaaelezwa kwamba waasisi hao wakasema hapana, na taarifa zinaeleza kuwa waliobuni na kufasiri amri zinazotumika jeshini wala hawakuwa na kiwango kikubwa cha elimu kama tulivyo wengi wetu 'waswanglishi' wa hivi sasa. Haidhuru hata kama walianza kwa kusema, 'nyumaaaaaazi geuka! kuliaaaaaaaaz geuka, mbeleeeeeeeee tembea!'shotu kulia, shotu kulia, shotu kulia!!! Mwisho wa siku Kiswahili kimetamalaki jeshini kwa kiwango kizuri kabisa.

Wakati umefika kwa viongozi wengine kukienzi Kiswahili kwa kukitumia, hususan katika hotuba zao ndani ya nchi. Bungeni ndiyo kabisaaaa.

Changamoto kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa

Balozi zetu nje ya nchi zianzishe vituo vya kufundishia Kiswahili kama vile zifanyavyo balozi za Ufaransa na Uingereza na nchi nyingine. Balozi zetu zifanye au zizidishe juhudi za maksudi kukitangaza Kiswahili, hata kama hakutakuwa na anayesikiliza, lakini na tufanye hivyo.

Balozi zetu zifanye kasi kubwa zaidi kuzishawishi taasisi za elimu kwenye nchi wanakotuwakilisha ili zianze kufundisha lugha ya Kiswahili, na wakati huo huo ziwe na orodha na mawasiliano ya vijana waliohitimu katika lugha hii ili wakihitajika tu, basi waweze kuwapata kirahisi. Tanzania tuendelee kuwa ‘wamiliki’ wa Kiswahili!!!

Mungu kibariki Kiswahili. Mungu tubariki Watanzania.

Wednesday, September 16, 2009

WASEMAVYO WENZETU KUHUSU KISWAHILI!!

Tazama maneno yaliyotiwa wino mzito.
Students looking to fulfill foreign language credits or who are interested in attaining an unusual minor now have a new option: Swahili.

In the spring and fall 2010 semesters, K-State will offer two new advanced courses in Swahili — Swahili III in the spring and Swahili IV in the fall. These courses are in addition to the two beginning courses already offered through the department of modern languages.

Robert Corum, professor and head of the department, said the new courses have been established in conjunction with the African Studies center.

“If we’re going to be an international university, we need to offer a wide variety of experiences and languages,” Corum said. “The addition of Swahili III and IV ... will prepare students for a more enriched experience studying abroad. It will also serve to be a good springboard for anyone planning on going to Africa.”

The Swahili language is to Africa what the English language is to America, he said. More than 150 million people speak the language in east and central Africa.

Swahili is the lingua franca,” said Geofred Osoro, K-State’s newly appointed Swahili instructor. “In other words, [it’s] the language of communication between countries and communities. There are many different languages in Africa, but everywhere you go, most likely the people will know Swahili.”

Because of this, Osoro, who spent his entire adolescent life in Africa before coming to the United States, said those who can speak the language will have greater ease in touring, exploring and researching in the country. Those who might benefit most from these courses, he said, are students planning to study abroad in Africa as well as students who need foreign credits to graduate with a bachelor of arts degree.

Swahili, while very different from the English language, does share some similarities, Osoro said.

“In Swahili, one word has many different meanings and is applicable to many things depending on context,” he said, much like the English language. “This makes it a challenge to students because one day this word means something, and the next day, it means something else.”

Swahili and English also use the same alphabet, Osoro said, which is at least one less worry when studying the language. The vowels, I, A, E, O and U, are the same in lettering, but always sound the same in Swahili, contrary to English.

“Think about toy and tool,” Osoro said. “In Swahili, it always stays the same, the ‘O’ sound. In English, it does not. And I promise you, Swahili is much easier to learn than English.”

Swahili I and II courses are currently available. Enrollment for Swahili III will start in the spring, and IV will be offered next fall.


IMEBEBWA KUTOKA http://www.facebook.com/note.php?note_id=134106904502&ref=nf

Monday, September 14, 2009

MCHANGO WANGU KWA SERA MPYA YA ELIMU NA MAFUNZO 2009

UTANGULIZI:
Kwa ujumla Sera mpya inashughulikia masuala muhimu na ya msingi kama vile kupunguza umri wa kuanza shule kutoka miaka saba hadi mitano; kuwekwa kwa utaratibu wa kuwatambua na kuwaendeleza watoto wenye vipaji maalum; kuanzisha polytechnics; kuongeza masuala ya TEHAMA na UJASIRIAMALI kwenye mtaala; pamoja na masuala mtambuka.

MAONI:

Kifungu Na 5.3 (elimu ya chekechea) Tamko Na. 4 na 5.4 (elimu ya awali) tamko la 3; na 5.5 (elimu ya msingi) tamko la 7 katika suala la ufanisi katika kutoa elimu bora ya msingi kwa wote na Tamko Na. 1 na 2 kwenye suala la kubaini na kuendeleza vipawa na vipaji vya watoto.

Matamko yote haya yanahusu kuwekwa kwa utaratibu wa kuwatambua watoto wenye vipaji katika vituo vya chekechea, madarasa ya elimu ya awali na shule za msingi kwa lengo la kuwaendeleza katika ngazi za juu. Hata hivyo nia hiyo haijaakisiwa kwenye kifungu 5.7 kichohusu Elimu ya Ualimu. Hapana budi kuwepo tamko la sera linalotilia mkazo kutolewa kwa mafunzo mahsusi kwa walimu (kazini na tarajali) katika ngazi zote kuhusu utambuzi na uhuishaji wa vipaji na vipawa vya wanafunzi. Hali kadhalika, tamko hilo lijumuishe umuhimu wa kuandaliwa kwa walimu ambao pia watakuwa washauri wa mieleko na kazi (Career counsellors). Ni dhahiri kuwa mafunzo ya hivi sasa yanayotolewa vyuoni hayakidhi haja hizi.

Pia hapana budi mfumo rasmi wa upimaji uwe na tamko juu ya kuwekwa kwa utaratibu utakao tilia mkazo na kusaidia uibuaji wa vipaji

Kifungu Na 6. 9 Utawala bora liongezwe tamko la sera lenye kuelekeza kuwa serikali itajuisha misingi ya utawala bora kwenye mtaala wa elimu katika ngazi mbali mbali ili kuwaandaa wananchi wenye fikra huru, wenye kujiamini, wazalendo na wawajibikaji na wenye kuhimiza uwajibikaji wa serikali na viongozi.

suala:Utoaji wa chakula kwa wanafunzi


Pamoja na sera ya elimu na mafunzo ya 1995 tamko la sera 3.2.7 kuainisha kuwa serikali itaboresha programu za lishe na afya katika shule za msingi na vyuo; upo ushahidi kwamba zoezi hili ambalo umuhimu wake umethibitika na kuthibitishwa kitaalamu kwa tafiti mbalimbali, halikuweza kufanikiwa sana. Tafiti mbali mbali zinaonyesha kuwa, mbali ya maeneo yenye programu za utoaji chakula zinazosaidiwa na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kama Dodoma, Singida na Manyara na Arusha, pia yale yanayosimamiwa na miradi ya kijamii kama baadhi za wilaya za mkoa wa Kilimanjaro n.k; maeneo mengine ya nchi hayakuweza kufanikiwa sana katika kutekeleza zoezi hili.
Watoto wengi hususan wanatoka familia maskini zaidi wameendelea kwenda shuleni bila chakula. Wengine wamekuwa wakitoroka na wengine kuacha shule kabisa. Badala ya kutamka kimkakati zaidi, sera mpya imelieleza suala hili kijuujuu tu kama suala la huduma muhimu shuleni na vyuoni (Ukurasa wa 68), ambapo tamko la sera linaelekeza jukumu la serikali kuwa ni kuhimiza wazazi, jamii, serikali za mitaa na wadau wengine kuhakikisha kuwa huduma ya chakula bora......

Pendekezo
Liongezwe tamko la sera kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau itaanzisha mpango kabambe wa utoaji chakula bora kwa wanafunzi wa shule za msingi wawapo shuleni ili kuwavutia kubaki shuleni na kuhakikisha wananufaika ipasavyo na matendo ya kujifunza.

Suala: usawa wa kijinsia:

Tamko Na. 6 kuhusu kuwekwa utaratibu wa kuwawezesha wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito kuendelea na masomo baada ya kujifungua; halina budi kukamilishwa na tamko jingine lenye kuelekeza kuwa serikali itaifanyia mapitio sheria ya elimu na kuelekeza namna ya kuwabana watu wanaowapa mimba watoto wa shule na kudhibiti mazingira yanayopelekea watoto wa shule kupata ujauzito.

suala:makundi yenye mahitaji maalum.
kuwepo na tamko kuwa serikali itaelekeza utaratibu wa kuandaa mazingira rafiki, ikiwemo ujenzi wa miundombinu rafiki kwa wanafunzi na walimu wenye ulemavu mbali mbali

Suala:ufundishaji wa lugha: ukurasa wa 77
Kufuatia maelezo kuwa Kiswahili ni lugha adhimu ambayo nyumbani kwake ni nchini Tanzania hapana budi kuitazama lugha hii kuwa na hadhi zaidi ya kiingereza. Lugha ya Kiswahili ni tunu ya kipekee kwa nchi zaidi ya au sawa na mlima Kilimanjaro. Kiswahili ni miongoni mwa raslimali ambazo Tanzania inaweza kuzipeleka duniani katika dunia ya kitandawazi kwani imezidi kukua duniani.

Licha ya kigugumizi cha kuamua kuwa na lugha moja ya kufundishia nchini (KISWAHILI) Kuwepo na tamko la sera lenye kuelekeza kuwa wizara yenye dhamana ya elimu kwa kushirikiana na wizara nyingine kama yenye dhamana ya utamaduni na ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa itatoa maelekezo ya kukipa Kiswahili kipaumbele kama raslimali ya kipekee, kuikuza na kuitangaza, ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya wahitimu mahiri wa lugha hii na kuendesha kampeni kabambe ya kuiingiza kwenye ulimwengu wa TEHAMA.

Suala: mfumo wa michepuo

Ukurasa wa 28 Tamko Na. 1 kuhusu kupanuliwa na kuendelezwa kwa utaratibu wa michepuo ya kilimo, biashara, ufundi na sayansi kimu.
kwa kuzingatia kuingizwa masuala ya TEHAMA na UJASIRIAMALI sambambaa na masuala mtambuka kwenye mitaala/mihtasari, ni vema sera itamke wazi kuwa itaifanyia mapitio mitaala ya masomo ya mchepuo (kilimo, biashara nk) ili kuifupisha na kuifanya iwe ya kivitendo na kijasiriamali zaidi au ikazie maarifa na stadi zinazopatikana kwenye mafunzo ya ujasiriamali. Vinginevyo hakuna faida kuwajazia wanafunzi mambo mengi ambayo hawataweza kumudu kuyashika.

Karibu tuchangie.

Saturday, September 12, 2009

HIV therapy could be given safely without routine laboratory tests to save more lives in Africa

HIV therapy could be given safely without routine laboratory tests to save more lives in Africa
Taking blood samples (Image from MRC DART Trial video) : Click to enlarge

The largest clinical trial of anti-retroviral therapy (ART) for people with HIV infection ever run in Africa has found that regular laboratory tests offer little additional clinical benefit to populations when compared to careful clinical monitoring. If lab tests are not routinely used to monitor the effects of ART, this means that many more people with HIV in Africa could be treated for the same amount of money.

The Development of Anti-Retroviral Therapy in Africa (DART) clinical trial, funded by the UK Medical Research Council (MRC), the UK Department for International Development (DFID) and the Rockefeller Foundation, aimed to find out whether the lab-based strategies used to deliver ART to people with HIV infection in resource rich countries were essential in Africa, where around 4 million people still need ART urgently and resources are limited. The trial, which began in 2003 and finished in 2008, involved 3316 people infected with HIV in Uganda and Zimbabwe.

DART participants were randomly allocated to one of two groups. People in the first group received ART and their doctor was given the results of blood tests done every three months to check for drug side-effects and measure their CD4 cell count (a measure of how well the immune system, which is damaged by HIV, is working). People in the second group had the same ART and the same blood tests done, but their doctors did not see CD4 count results and only saw the results of safety tests if they were seriously abnormal. People in both groups received free medical care and free diagnostic tests for episodes of illness throughout the trial.

Speaking about the results of the trial, co-principal investigator Professor Diana Gibb of the MRC Clinical Trials Unit in London said: "The survival of people who took part in the trial was remarkable; without treatment only about 10% of HIV-infected African people like those in DART would be expected to survive for five years. In DART, 87% of those receiving treatment without routine blood test monitoring were still alive and well after five years, only 3 percentage points less than in the group that had routine blood test monitoring. For health policy-makers in Africa, DART provides evidence that more people could be treated for the same amount of money by not using routine laboratory tests. This would substantially reduce the number of people dying with serious disease due to HIV infection. "

DART co-principal investigator Professor Peter Mugyenyi of the Joint Clinical Research Centre in Uganda said: "It is estimated that two-thirds of people who need treatment for HIV in Africa currently don’t have access to antiretroviral therapy. Thanks to DART, Governments now have evidence that expensive blood tests aren’t needed routinely for HIV treatment to be successful and safe. It also means that treatment could be delivered locally as long as health care workers have the right training, support and supervision. This could make a huge difference to people who live in remote areas that are many days’ walk from the nearest hospital or laboratory. "

International Development Minister, Mike Foster of DFID said: "It’s absolutely clear that anti-retroviral treatment saves lives – but the cost of accompanying laboratory tests significantly reduces the number of people that this treatment can reach. The DART trial, for which DFID provided £2.5m in funding, shows that this life saving treatment can still be safely provided without this additional cost. "

"Crucially, the money saved from paying for these tests could enable more people to safely receive treatment, including those who for whatever reason are unable to travel to the laboratories. Such a step would be an important move towards our ultimate aim of achieving universal access to treatment for HIV/AIDS by 2010. "

More information

* For more details, and additional quotes from other co-principal investigators, please read the full MRC media release.
* Watch the YouTube video clip about the trial on the MRC YouTube channel.
* The results of the DART trial were presented at the 5th International AIDS Society (IAS) Conference on HIV Pathogenesis, Treatment and Prevention, held in Cape Town, South Africa, on the 19-22 July 2009. For the DART presentations made at the conference please see the DART website or the outputs attached to the project record giving details of DFID's support to DART.

source:
http://www.research4development.info/news.asp?ArticleID=50487

Wednesday, September 9, 2009

RAIS WA WATU ALIPOZUNGUMZA NA WANANCHI

Naam tarehe 9.9.09 Rais kazungumza na wananchi kwa kujibu 'maswali yao'. Hakika Rais wetu alikuwa na bahati saana kuulizwa maswali kuhusu masuala ambayo Rais yeyote wa watu angepennda kuyazungumza kwenye hotuba yake, hata kama hakuulizwa na wananchi wake 'wanaompenda sana.'

Suala la kuziba midomo watu kwenye vikao vya chama chake, suala la mikoa iliyopembezoni, suala la ufisadi, suala la mtikisiko wa muungano, nyaraka za madhahebu ya dini nk ni masuala yanayosumbua nafsi za watu, na kwa kweli wauliza maswali walilenga!!!!!!

Yaliyonigusa:
Rais 'anaijua' tanzania kweli kweli maana ameweza kuzungumzia barabara zinazojengwa kwa urefu, kiasi cha pesa, mkandarasi, nk utadhani waziri wa ujenzi!!Rais amezungumzia takwimu za elimu mwaka kwa mwaka, mwaka hadi mwaka utadhani waziri mwenye dhamana ya elimu, au hata zaidi yake. Hakika mheshimiwa rais ALIJIANDAA. CONGS

Kwa kusikiliza na kutafakari majibu ya rais kuhusu nyaraka na miongozo ya madhehebu ya dini nashindana na nafsi yangu kuamini kuwa 'Waislam', na askofu Kakobe walipangwa au walitumwa kuyazungumzia kwa mtindo wa Yohana mbatizaji. Hajaeleza kwa kina mathalan, ni vipi waraka wa katoliki unakuwa issue ya kuhatarisha amani, maana hauelekezi dini ya mtu wa kuchaguliwa. hajaeleza kwa kina hofu inatoka wapi?

Rais walau ametueleza kwa kina kuhusu kikao cha CC na NEC ya CCM na kutuahidi kuwa kwa nafasi yake ya uenyekiti wa chama hicho HATARUHUSU WATU WAZIBWE MIDOMO, na kwa mtazamo huo ataendelea kusimamia wajibu wa wabunge wa chama hicho kwa wananchi zaidi si matakwa ya chama chao pekee.

Hata hivyo mwenyekiti huyo wa CCM hakuzungumzia ni Mshindani wa Spika wa sasa kwenye kinyang'anyiro cha nafasi hiyo, yaani Msekwa awe mmoja wa wazee wa kutafuta ufumbuzi wa mkanganyiko ndani ya chama, Je CCM imeishiwa wazee?

Kuhusu ufisadi, pamoja na kuwa amejitahidi kuzungumzia kuandaliwa kwa mfumo wa kisheria wa kuwabana mafisadi, hajaeleza mathalan kuhusu tuhuma za mapambano ndani ya chama hicho, ambapo baadhi ya vigogo wanatuhumiwa kutumia mijihela kuwakandamiza wenzao.

Tuesday, September 8, 2009

RAIS WA WATU KUZUNGUMZA NA WANANCHI

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120 ,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kesho, Jumatano, Septemba 9, 2009, atazungumza moja kwa moja na wananchi kupitia Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na vyombo vingine vya utangazaji nchini kuanzia saa mbili na nusu usiku. Mbali na TBC, televisheni nyingine za ITV, TVZ, Mlimani TV, Tumaini TV na Channel Ten zinatarajia kuonyesha mazungumzo hayo.

Rais atatumia aina mpya ya kuwasiliana na wananchi kwa kusikiliza hoja zao, kwa kujibu maswali yao , kusikiliza ushauri wao na kupata maoni juu ya mambo yanayohusu mustakabali wa nchi yetu, Serikali yetu na maendeleo yetu.

Aidha, Rais atasikiliza matarajio ya wananchi katika jitihada zao za kuboresha maisha yao kwa kujiletea maendeleo.

Mazungumzo hayo yatakayochukua muda wa dakika 90 kuanzia saa mbili unusu usiku (saa 2:30 usiku) hadi saa nne kamili usiku.


Aidha mazungumzo hayo yatatangazwa kwenye redio za TBC-Taifa, Sauti ya Tanzania, Zanzibar, Radio Mlimani, Radio Clouds, Radio Tumaini, na Radio Uhuru.

Maswali, maoni, hoja, ushauri utapokelewa moja kwa moja na TBC kupitia simu nambari +255-22-2772448, +255-22-2772452 na +255-22-2772454.

Aidha, maswali, maoni, hoja ama ushauri unaweza kutumwa moja kwa moja TBC kupitia ujumbe mfupi wa SMS kwenye nambari 0788-500019, 0714-591589 na 0764-807683 ama kupitia kwenye barua pepe swalikwarais@yahoo.com kuanzia leo.

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais inawashauri wananchi kutumia kikamilifu nafasi hiyo ya kuwasiliana moja kwa moja na Rais wao.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

08 Septemba, 2009

CHANZO:
www.wanabidii.net

Monday, September 7, 2009

RUNGWE YAPIGA HATUA KUIMARISHA UTAWALA BORA





















































Kuimarisha utawala bora ni mchakato endelevu. Katika kutimiza hilo, Halmashauri ya wilaya ya Rungwe imepiga hatua kwa kuweka 'ubao' wa matangazo uliorafiki kwa watumiaji. Sifa bainifu za ubao rafiki ni pamoja na kuwa na sehemu z aidi ya moja na kutumiwa kuweka matangazo si tu na utawala bali watumia huduma pia (interactive); na kuwekwa mahali panapofikika kirahisi bila hofu na wakati wowote. Halmashauri ya wilaya ya Rungwe imeondosha ubao wa matangazo kwenye ukuta wa ofisi za halmashauri hiyo na kujenga katika eneo la wazi zaidi na linalofikika karibu wakati wote. Hatua hiyo haina budi KUPONGEZWA. Hata hivyo wadau hawanabudi kuzingatia kwamba KUWEKA miundo mbinu ni hatua moja na KUITUMIA yaweza kuwa jukumu tofauti kabisa.


SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP