Pekua/search

Thursday, May 8, 2008

Mfano rais Truman kwa Wanasiasa wa Bongo

Amani iwe nanyi.
Na kwa yakini, mheshimika Truman alikuwa sahihi. Hakuna tofauti kati ya kazi mbili alizochagua; uanasiasa na upiga mziki kwenye 'danguro,. Ndiyo maana Mh. Lower sir na Chen ge wanaibuka mashujaa majimboni mwao na katika chama chao (kwa viongozi wa chama kuwaandalia mapokezi mazito, kana kwamba wametoka vitani!) na upande wa pili Dkt. Mwakyembe, alizuiwa na viongozi wa chama chake (wa ngazi sawa na wale wanaoandaa mapokezi kwa watajwa hapo juu) kushiriki maandamano yaliyoandaliwa na wananchi kumpongeza na kumfariji baada ya kutijotaa mhanga na 'kujilipua' bungeni. Uongozi wa CCM mkoa wa Mbeya uliripotiwa kujaribu kumzuia asishiriki mapokezi ya wananchi kwa madai ya maelekezo kutoka ngazi za juu za chama hicho. Sasa sijui na mapokezi ya kina Lowasa na Chenge, ni maelekezo ya CCM ngazi za juu??? JE BADO CCM NI MOJA?? JE CCM BADO KIPO?

Wenzetu mnaokuwepo kuushuhudia 'utitiri' wa watu kwenye mapokezi hayo, tujuzeni, MWAANDAAJI NI NANI??? Haitoshi kutuambia kwenye vyombo vya habari kuwa watu walifurika kumpokea shujaa 'pengine wa kifisadi'. Twambie jamani, iliitwa na nani kadamnasi hiyo? Kama watu walizuka tu kama madume ya mbwa yamtokeavyo mbwa jike aliyetayari kupandwa, napo mtwambie. Kama wananusa tu, kuwa shujaa wao anashuka eapoti saa fulani na haraka haraka wanajikusanya kama tai wauzongavyo mzoga, si vibaya tukaambiwa pia.

Hata Kama mhusika, ndiye anayeandaa ili kupata fursa ya kuwagawia vijisenti vya 'kifisadi' wapiga kura wake, napo tuambiwe ati!!TUJUE,kwani TUSIJE PIGA KELELE KUMBE WANAJIMBO na CHAMA HUSIKA NDIYO WALIOWATUMA WAHESHIMIWA HUSIKA KUIFISIDI NCHI, NA NDIPO BAADA YA MAFANIKIO WANARUDI MAJIMBONI KUSHEREHEKA NA WATU WAO!!TUJUE MUKTADHA WA MATUKIO HAYA KUTOKA PANDE ZOTE. KUTUAMBIA MHESHIMIWA ALIVAA SUTI GANI, TAI NDEFU AU FUPI, ALIONGOZA NA MKEWE AU KIMADA, BI MKUBWA AU MDOGO,(kama msomi mmoja alivoandika habari za lowasa) HAITUSAIDII SANA.

WANASIASA WATU WAAJABU. Mathalan, si ajabu Chen ge, ALIJIUA maksudi ili apate agenda ya kutambia jimboni kwake. "Mnyantuzu hawezi kujiua aache vijisenti vyake" ndivyo yalivyo mnukuu magazeti ya leo. Kwa hiyo yaweza kuwa yeye na wapendwa wake, alipanga maigizo haramu. Akajiua. akaonewa huruma. akageuza mjadala, Dar hadi jimboni kwake, na Tanzania nzima. Hoja kwa wapiga kura wake, imekuwa si kutuhumiwa ufisadi, bali kuzushiwa kifo!!!Kutotakiwa mema.Kuandamwa kisiasa. (NANI ANAMWANDAMA? KISA NINI? WAMEANZA LINI KUMWANDAMA? YEYE KAWAANDAMA WANGAPI?). SIASA BWANA!!!

CHENGE anakwenda kwa wapiga kura wake kuwaambia yaliyomtokea ni nasema NI AJALI YA KISISA!! Hii ni dharau ya hali ya juu. je hii si kejeli ya mara ya pili kwa JK baada ya kuwajibu jeuri waandishi, "KAMUULIZENI ALIYENITEUA" . Sasa anakariri maneno ya JK huyo huyo, alipokuwa akijaribu 'kumtetea' swahiba wake Lowasa mbele ya wazee wa jiji la Dar es Salaam.(Lakini wacha JK AKOME!!MAANA UKING''ANG'ANIA KUBEBA ZIGO LA MAVI, LAZIMA UKOME. HARUFU YAKE SI MCHEZO, ATI!!)Wacha JK anyooshwe!! kwani maandiko matakatifu yanabainisha, "MTU AKISHUPAZA SHINGO, HUVUNJIKA GHAFLA"

WALAU, CHENGE angejitetea kwa wapiga kura wake kwa kueleza alivyopata vijisenti vyake (hana haja kusubiri SFO wampe madokezo), na ni kwanini ameviweka nje ya nchi kimya kimya, wakati hata Bariadi au Shinyanga benki zipo (na kama hazipo vijisenti hivyo vingeweza kusaidia kuwa mtaji wa benki ya 'wanyantuzu' ! Sasa anaenda jimboni kupeleka kejeli!!. AMA KWELI, 'MUNGU HUWAPIGA UPOFU WENYE DHARAU, MAJIVUNO NA KIBURI'.

SIJARIBU KUMHUKUMU CHENGE, LAKINI HAKIKA NI AFADHALI KUSIKILIZA wimbo "Jini jini anipenda sana, anasema ananipenda.. . au hata zaaaaali la mentali..ama mabinti wa kitanga na kujipamba kwao" tukaburudisha nyoyo, KULIKO KUSIKILIZA porojo zake CHENGE na nduguze.

AHSANTE NDUGU KISINDA KWA KUMUVUZISHA KA INSIGHT HAKA KUHUSU MAISHA YA MODO TRUMAN. I COULDNT RESIST IT THIS MORNING, SASA WALAU, NAWEZA KUENDELEA NA KAZI.TRUMAN IS TRULY A GREAT INSPIRATION! !!!

Adam, L

--- In wanazuoni@yahoogrou ps.com, Mgune Masatu wrote:

Fewer are like Him.

Octavius Kisinda wrote:
FYI

Harry Truman....proof that there is some good men in the World.......

Harry Truman, Former President of US When President Truman retired from office in 1952, his income was substantially a U.S. Army pension reported to have been $13,507.72 a year. Congress, noting that he was paying for his stamps and personally licking them, granted him an "allowance" and, later, a retroactive pension of $25,000 per year.

When offered corporate positions at large salaries, he declined, stating, "You don't want me. You want the office of the President, and that doesn't belong to me. It belongs to the American people and it's not for sale."

Even later, on May 6, 1971, when Congress was preparing to award him the Medal of Honor on his 87th birthday, he refused to accept it, writing, "I don't consider that I have done anything which should be the reason for any award, Congressional or otherwise."

We now see that the Clintons have found a new level of success in cashing in on the presidency, resulting in untold wealth. Today, many in Congress also have found a way to become quite wealthy while enjoying the fruits of their offices. Political offices are now for sale.

Was good old Harry Truman correct when he observed, "My choice early in life was either to be a piano player in a whorehouse or a politician. And to tell the truth, there's hardly any difference".

NB: I, for one, believe the piano player job to be much more honorable than current politicians. What do you say????

Source: wanazuoni yahoogroup

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP