Pekua/search

Friday, June 13, 2014

Mr. Taxman: What have you done for me lately?



 Je Huduma zitolewazo na Serikali zinaendana na Kodi kubwa na nyingi?
Waziri wa Fedha, Saada Salum Mkuya

Uhalali pekee wa serikali kutoza wananchi wake kodi kubwa na nyingi unatokana na huduma zinazotolewa na uwajibikaji wa serikali kwa wananchi katika kujibu hoja na madai yao kuelekea huduma bora na kurekebisha kasoro (Obligation to provide explanation and take corrective measures). Sasa hapa kwetu Halmashauri inaweza kuwa na hati chafu hata miaka mitano mfululizo lakini hakuna maelezo ya kutosheleza wala hatua madhubuti kurekebisha hali hiyo.

Kati ya bajeti ya trilioni 19.8 ni bilioni 6.3 tu ndio za miradi ya maendeleo. Hizi trilioni 13 na upuuzi juu zinaenda wapi? NI matumizi ya kawaida yakiwemo nay ale yanayosababisha tuletewe mitandaoni picha za NYUCHIz.

Wasanii Lucky Dube na Masudi Kipanya wameeleza yote. Fuatilia. Jihoji pamoja nao.
Taxman wa Lucky Dube.

I pay my gardener to clean up my garden

I pay my doctor to check out da other ting
I pay my lawyer to fight for my rights
And I pay my bodyguard to guard my body
There's only one man I pay
But I don't know what I'm paying for
I'm talking about the taxman
I'm talking about the taxman
I'm talking about the taxman


What have you done for me lately
Mr Taxman
What have you done for me lately
Mr Taxman
What have you done for me lately
Mr Taxman
What have you done for me lately
Mr Taxman


You take from the rich, take from the poor
You even take from me, can't understand it now
I pay for the police to, err...I don't know why
'Cause if my dollar was good enough
There wouldn't be so much crime in the streets
They tell me you're a fat man
And you always take and never give

What have you done for me lately
Mr Taxman



Jikumbushe wimbo wa Dube TAXMAN Bonyeza HAPA

https://www.youtube.com/watch?v=Vv6AQHKceBA  

Vibonzo na picha ya Waziri Saada ni kutoka

Monday, June 2, 2014

Buriani Mwanaharakati Bi Shida Salum



Buriani Mwanaharakati Bi Shida Salum

Safari ya Shida Salum katika dunia hii iliyojaa dhiki na simanzi imefikia tamati. Amepumzika sasa. Kadri historia ya Taifa hili inavyoandikwa upya Watanzania tutamkumbuka kwa mengi. 

Hakika Shida Binti Salum alizivaa na kuzimudu kofia nyingi. Alikuwa mzazi, mwanasiasa na mwanaharakati. Wapo wanaomjua zaidi kama mzazi. Pia wapo wanaomfahamu zaidi kama mwanasiasa. Tupo na tunaomtambua zaidi kama mwanaharakati.

Nilikutana naye kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2006 wakati tuliposhirikiana katika utafiti wa taasisi ya HakiElimu kuhusu haki ya kupata taarifa/habari. Alikuwa akitokea kwenye mtandao wa asasi zisizo za Serikali za Kigoma na Kasulu unaojulikana kama Kigoma and Kasulu Non-Governmental Organizations Network (KIKANGONET). Wakati huo sikuwa namfahamu mtoto wake, Zitto Kabwe, ambaye nilikuja kumsikia kwa mara ya kwanza mwaka 2007 baada ya wanaharakati wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kuandaa maandamano ya kumuunga mkono katika viwanja vya Mabibo kufuatia kutolewa kwake nje ya ukumbi wa Bunge baada ya kuibua tuhuma nzito kuhusu ufisadi wa Mgodi wetu wa madini wa Buzwagi. Kwa lugha tunduizi ya Kifeministi, hii ina maana nilimfahamu Shida kama yeye - Shida Salum - kabla ya kumfahamu kama Mama Zitto kwa kuhusianishwa na umaarufu mkubwa aliojizolea mwanae katika medani ya kisiasa nchini.

Tunapomkumbuka Shida kama mzazi aliyemlea mwanasiasa mashuhuri pia tusisahau kumkumbuka kama mwanaharakati mahiri aliyeendesha harakati na wenzake kama yeye na kupata ukubali katika jumuiya za wanaharakati kama yeye na si (tu) kama mzazi wa fulani. Katika harakati za kutafuta haki ya kupata taarifa, alishiriki kudhihirisha kiutafiti ni jinsi gani watu wa kawaida, wakiwamo wenye ulemavu, wanakosa fursa ya kupata taarifa muhimu kwa ajili ya umma. Cha kusikitisha ni kuwa hata taasisi zisizo za kiserikali ambazo zinajiona ziko kiharakati zaidi na bora kuliko taasisi za kiserikali nazo hazikuwa mstari wa mbele katika kutoa taarifa muhimu kwa wananchi pale wanapofika kwenye ofisi zao au hata kutuma maombi kwa barua ama kwa kupiga simu.

 Katika harakati huyu ndiye Shida tuliyemfahamu. Mwombolezaji mmoja katika mtandao wa Wanazuoni aliyewahi kufanya kazi katika taasisi ya HakiKazi anamkumbuka hivi: 

"Nilimfahamu Bi Shida Salum kama Mwanaharakati tokea Kigoma na kisha hapa Dar na Dodoma kwenye harakati zake za kutetea Watanzania wenye ulemavu na maendeleo kwa ujumla. Ameacha legacy." 
 Hii "legacy" yake, ama kumbukumbu ya kupigiwa mfano kwa tafsiri ya haraka haraka, tuienzi katika harakati za kuyafanya maisha ya kila Mtanzania - mdogo ama mkubwa, mwenye ulemavu au asiye na ulemavu, mwanamke na mwanaume - yawe bora (zaidi na zaidi).

Nilipomkuta amekaa mbele ya banda alilokuwa akilisimamia katika maonyesho pale katika Viwanja vya Mnazi Mmoja sikujua kuwa hiyo ndio itakuwa mara yangu ya mwisho kuongea naye. Shida niliyemkuta hospitalini AMI, japo hatukuongea, sauti yake bado ilikuwa ya mwanaharakati asiyekata tamaa, akipambana vikali na moja ya vile ambavyo mmoja wa waasisi wa Taifa letu changa la Tanzania aliviita maadui (wakuu) watatu wa maendeleo (yetu).

Ingawa hatutamsikia akipaza sauti yake mwenyewe katika Bunge Maalum la Katiba na maeneo mengine akiwakilisha kundi la wenye ulemavu, sauti hiyo itasikika kupitia wale aliowaachia makabrasha au waliompokea kijiti. Lakini tusiwaachie tu kina Fredrick Msigallah jukumu nyeti la kutetea na kudai haki hizi ambazo, kwa namna moja au nyingine, zinatuhusu hata na sisi ambao hatuna, ama tunaojiona hatuna, ulemavu. Na moja ya haki (za kiraia) za watu walio na ulemavu ni kushiriki kikamilifu katika siasa kwa maana ya kuongoza, kuwakilisha, kupigiwa na kupiga kura n.k.

Maisha ya Shida ni kielelezo tosha kuwa mwanamke mwenye ulemavu anaweza kuwa mzazi, mwanasiasa na mwanaharakati. Tunapojiandaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 tukumbuke pia kurekebisha masuala tete na tata yaliyoibuliwa na utafiti huu wa CCBRT kuhusu changamoto za ushiriki wa watu wenye ulemavu katika uchaguzi wa 2010 ambao kwa kweli ulinifungua sana macho. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaenzi harakati zake.


Kigoma mpokee mwanao. Binti wa Tanzania. Mtoto wa Afrika.

Buriani Shida Binti Salum.

Imeandikwa na Mwanazuoni Chambi Chachage http://udadisi.blogspot.co.uk/2014/06/buriani-shida-binti-salum.html

Naam Nenda Mwanaharakati Shida Salum. Umemaliza safari https://www.youtube.com/watch?v=mrxFySY45wc

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP