Pekua/search

Saturday, April 26, 2008

AJALI - Njiro SDA Arusha. Kuna pepo hapa???

AJALI - Njiro SDA Arusha. Kuna pepo hapa???

AJALI HAINA KINGA??

Tigo Zanzibar Music Awards 2008. (Alhaj Goya)

Alhaj Goya.

popularly known for his song "Hali ya Pemba" which was reportedly 'censored' by Government 'authorities'; poses with his prize March this year.

some of the verses of Hali ya Pemba;

Hali ya Pemba miji isha fifia jamani,
Si Wete, Chake wala Mkoani
Miji haipo kama zamani,
Ni kwanini?

The towns in Pemba island is in shambles
Neither Wete, Chake nor Mkoani is any better
The towns are no longer like what they used to be,
why?

Karafuu za kwangu mwenyewe
Serikali wao ndo wanunuzi,
bei wao wenyewe wajipangia,
Wala hili zao halijanadiwa

The cloves are mine
The government the sole buyers
It sets the prices arbitrarily

Tuwekeeni maji na umeme wenye uhakika
Ili wawekezaji waje Pemba kuwekeza
Pesa mlizouza mmenunulia silaha?
Maana hizi tumeziona

We want reliable tap water and electricity
So as to attract investors to Pemba
Did you buy weapons with the money you got from our cloves?
Yes, we have seen the weapons!

Awamu iliyopita Zanzibar
Kwa Pemba ilikuwa mashaka
Huu ni ukweli usofichika
Ila umefichwa

The previous government phase
did nothing to Pemba
This is the naked truth
Only that some people are trying to hide it

Thursday, April 24, 2008

Tigo Zanzibar Music Awards 2008. (Baby J)


Baby J, the winner of this year's two prizes at the Zanzibar Music Award 2008, one as 'female upcoming artist of the year', and one as 'female artist of the year'

Baby J – real name: Jamila Abdallah Ally – is one of the promising young
zenji flavour musicians in Zanzibar. 'Zenji flavour' is what the Zanzibar youth calls their local style of hip-hop. .

Wednesday, April 23, 2008

Tigo Zanzibar Music Awards 2008. (The Akhenatons)


The Akhenaton Family, winners of the Best music group Award (Muziki wa kizazi kipya) in Zanzibar 2008, pose in a group picture after the Tigo Zanzibar Music Awards 2008 ceremony that was organised by Zenj entertainment . Friday 20th March 2008,


Akhenaton family, a group of youthful musicians in Zanzibar was founded in 2005 uniting young Zanzibari musicians (Kizazi Kipya). The birth of the family was spearheaded by David Murphy (DotCom) so as to create opportunities for the artists and increase team work and the integrity on the lyrics.

After a long struggle in music industry,
their song Amka Africa was first nominated in 2007 in Kenya Awards in the category ‘Best Video Tanzania’ but they were not successful.

In 2008 according to the airwaves and fans, Akhenaton Family is the only group in Zanzibar that has managed to create a relatively different sound, team work and performance after the release of their 2008 collection (Jibu, On the Air). They also work together with several talents within the isles and this has inspired a lot of youths to develop their talents through the Akhenaton family spells.

Saturday, April 19, 2008

Mama Salma Kikwete aigwe. (Mchango zaidi)


Ni kweli kabisa huu ni mjadala wa kudumishwa.. ..

KWANINI TBC - Tanzania broadcasting commision jamani
ilishindikana kuita SUT - Shirika la utangazaji
Tanzania.

Mimi hasa huwa najiuliza ni nini hasa na tatizo li
wapi maana naona kama sasa huu utaratibu wa nchi yetu
sijui unakoelekea.

Sawa watu wamekuwa mafisadi kupindukia inawezakana
walikuwa hivi toka zamani lakini sikuhizi ndio
tumefahamu ila hata kwenye lugha jamani lugha. Mie
naona itabidi tuanzishe utaratibu wetu wenyewe maana
mtu ukinyimwa haki yako inabidi uichukue hii lugha
yetu kwanini isipewe nafasi yake.TUTUMIE KISWAHILI
KADRI TUTAKAVYOWEZA.

Naomba kuwasilisha
From:
To:
wanazuoni@yahoogroups.com

RAISING VOICES, NO FAVOUR, IT'S A RIGHT


Traditionally women among the Maasai are reported to have been greatly marginalized. For example, they were not allowed to stand up and speak their concerns in a meeting. If the issues is that pressing, a woman had to support herself on her knees as sign of respect for men (and stand up like men do), then she could humbly speak.

However, Ngodi (pictured right) said things were getting better. "We demand our rights. We can now speak whether they like it or not.Its our right." Said Ngodi in Lobbying and Advocacy Training at Namanga. The training was organized by MVIWAMO (a net work for small farmers and pastoralists' groups in Monduli & Longido)

Photo by Adam, L

Friday, April 18, 2008

Mama Salma Kikwete aigwe. (Mchango zaidi)

Mjadala huu ni muhimu na hauwezi kufungwa kirahisi bila nasi wengine kutia timu.
Historia inaonyesha kuwa inahitajika utashi wa Kisiasa katika kuifanikisha hilo. Naomba ifahamike kuwa, hata Kiingereza kutumika kama lugha rasmi haikuwa rahisi kama tunavyofikiria. Kuna Wanazuoni, Maprofesa wa vyuo vikuuu walijiuzulu kwa kuwa tu Kilatini kilisitishwa kama lugha rasmi ya mawasiliano na kujipatia maarifa. Watu walikiona Kiingereza kuwa na mapungufu makubwa katika kujifunza na kwamba hakikuwa na misamiati ya kutosha kama ilivyo Kiswahili pengine kwa leo.
Lakini kwa upande mwingine naomba niwakumbushe kuwa lugha kama lugha inapitia hatua mbalimbali mithili ya kiumbe hai. Hivyo kadiri ya mahitaji na misamiati mipya, ndivyo itakavyotoholewa kwa kadiri ya mahitaji ya jamii na hatimaye kuwa na maneno maalumu. Hatupaswi kukata tamaa na kama neno halipo ina maana kuwa katika jamii hiyo hicho kitu hakifamiki. Endapo kitafahamika kitapewa jina.
Je, leo hii ni nani wanaongea na kutumia Kilatini kama lugha rasmi? Sina hakika kama kuna nchi zaidi ya Vatikano ambayo inakikubali na kukitumia Kilatini kama lugha rasmi katika mawasiliano na kufanyiwa tafsiri katika lugha mbalimbali. Lakini haina maana kuwa Kilatini hakipo na kwamba hakitumiki.
Ukipenda kitu chako utashawishi na wengine pia wakipende na kukutumia ndivyo utakavyoshawishi na wengine pia.
Inawezekana, timiza wajibu wako!

KISINDA,Octavius Alex
P O Box 13547
Dar es Salaam
Tanzania,The United Republic

Chanzo: Wanazuoni yahoogroup

Siyo mafunzo ya KARATE; Ni Kupasha tu!!


Baada ya majadaliano na kushirikishana ufahamu, maarifa na ujuzi kuhusu mapendekezo ya MKURABITA juu ya urasimishaji wa mali na biashara, huko Matema, Kyela mkoani Mbeya pichani washiriki wakiongozwa na mwenzeshaji (Adam, L) 'wakipasha' kwa kunyoosha viungo.

Kujifunza kunapaswa kuwa tendo linalofurahiwa.

Thursday, April 17, 2008

Mama Salma Kikwete aigwe. (Mjadala zaidi)


Mjadala huu hautafikia ukomo maana hata ufanyike utafiti wa namna gani unaohakikisha tena na tena na tena kwamba watu huwa bora zaidi wanapojifunza, kuwasiliana au kutumia lugha zao za kwanza, ukweli utabaki kwamba dola za magharibi zinazotumia lugha ya kiingereza bado zinatawala utamaduni wa kizazi kipya. Na si wote walioweza kujikomboa toka kwa kasumba ya ubora wa magharibi kwamba kuendelea, kuelimika na kustaarabika ni kuachana na asili zetu na kukumbatia umagharibi katika utamaduni hasa katika lugha.

Ni kweli kwamba katika dunia ya sasa ya utandawazi, kujua lugha za kimataifa kama kiingereza kuna manufaa zaidi. Ila lugha hizi zinatakiwa ziwe nyongeza siyo badala ya lugha za asili. Msisitizo lazima uwe kwa lugha ya kwanza na baada ya hapo mtu akijifunza lugha ya ziada, vyema.

Kwetu sisi uzalendo ni kuvutiwa na kuwaunga mkono watu wanaofanya juhudi kukuza kiswahili, bila kujali sababu zinazopelekea mapenzi yao na ustawi wa kiswahili.

Binafsi huwa nafurahishwa sana na viongozi wa nchi za kiarabu hasa raisi wa Misri wanavyopenda lugha zao na kuzitumia hata wanapokuwa katika mikutano na viongozi wa magharibi. Mojawapo ya mikutano hiyo katika Ikulu ya raisi wa Marekani, Hosni Mubarak akaanza tu hotuba yake kwa kiarabu huku inarushwa moja kwa moja na unaona nyuma maafisa wakihangaika kutafuta mtafsiri ila yeye hata hakusubiri apatikane akaendelea tu na hotuba yake. Hawa ni viongozi wachahce wenye ujasiri wa kutetea tamaduni zao kwa gharama ya kuonekana malimbukeni kwa watu wao wenyewe kama baadhi yetu wanavyomuona Salma.


To: wanazuoni@yahoogrou ps.com
From: ericbeda@gmail. com
Date: Thu, 17 Apr 2008 11:03:54 -0400
Subject: Re: [wanazuoni] JUU YA LUGHA

Wanazuoni,

Mjadala wa Lugha kama msukumo wa elimu na maendeleo imeshafanyika sehemu nyingi sana duniani na utafiti nyingi zilizofanywa zinaunga mkono wa kuwa kusoma au kutoa/kupokea elimu kwa lugha yako ya kwanza inasaidia kwa kiasi kikubwa kukuwa kwa uerevu wa mtu haswa kwa watoto chini ya miaka 14.

Sababu ya sisi watanzania kutokuthamini lugha yetu au kutokutumia lugha yetu katika mitaala yote na ngazi zote za elimu bado ni kitendawili kwangu mimi ila nadhani hizo sababu zinaweza kufanana na sababu za ingawa nchi za ulaya zinatoa ruzuku kwa wakulima wao sisi watanzania hatutowi(au haturuhusiwi kutoa) ruzuku kwa wakulima wetu, na ingawa kilimo kilikuwa (sina uhakika tena) kinachangia asilimia 80 ya uchumi wetu mitaala yetu elimu ya msingi ilibadirishwa (nadhani imeshawekwa sawa) na sayansi kilimo kikafutwa


On Thu, Apr 17, 2008 at 8:42 AM, bernard baha <bahabp2003@yahoo. com> wrote:

Amani kwenu wanazuoni,
Huu mjadala wa lugha mimi nilidhani umefikia ukomo na wote sasa tunaelewa jinsi ambavyo kutumia lugha za watu inavyokuwa taabu kuyafikia maendeleo. Sasa kumbe kamaradi Adam na Dada Catherine wamenifungua macho kabisa kwa kuuibua huu mjadala. Ebu nirejee kwanza katika baadhi ya hoja za dada yetu mpendwa Catherine,kwamba isingekuwa wasomi tusingepata uhuru,nadhani hoja yake hapa ni umahiri wa Mwl kwamba aliweza kuwakonga mioyo Waingereza na kuwashawishi kwamba tupo tayari kwa uhuru!
Nadhani hii hoja haijitosherezi kabisa ktk utetezi wake, ama ndiyo kusema kama tukiinyambua kimantiki kwamba bila kiingereza Tanganyika ingeendelea kuwa koloni! huu ni upotoshaji wa historia yetu na nafasi ya lugha ya kiswahili katika kuleta uhuru wa Tanganyika,hicho kiswahili cha wandengereko, wazaramo, na makabila uliyoorodhesha ama kusema watu wa ukanda wa Pwani sio tena mali ya kabila ama kundi fulani kama lugha za makabila mengine! tupo wengi tuliozaliwa katika Tanzania ya leo ambao lugha yetu ya kwanza ni kiswahili na tunaota na kufikiri kwa lugha hiyo! Lugha ya kiswahili ndio lingua franka ya Afrika ya Mashariki na Kati kama ilivyokuwa Kiinglishi kwa Ulaya na maeneo mengineyo.
kusambaa kwa lugha ni juhudi na jitihada za wenye lugha kuisambaza na kujivunia kuitumia na hivyo kuwafanya wengine wasioitumia wafikirie kuitumia pia,sasa vitendo vyetu ndio vinatuponza tunaukimbilia uingereza na kuona aibu kutumia kilicho chetu matokeo yake ndiyo haya mpaka leo tunapiga jaramba hatusongi mbele kama Taifa kimaendeleo
Kama ambavyo wao wanajifunza lugha zetu kwa ajili ya matumizi hata sisi twaweza fanya hivyo hivyo kwa lugha zao huku tukiweka mbele zaidi matumizi ya lugha yetu,pale inapolazimu ndio tutumie lugha zao.Lugha ni utamaduni wa taifa sasa kwa kufikiri kizungu vp ndio tutakuwa kama wao ama? Ndio maana Frantz Fanon alituasa kama tunafikiri hatujawa tayari kujitawala na kama tunaona kwamba Ulaya ama Uingereza ndio kwenyewe tusipoteze muda tuwalete Waingereza warudi kututengeneza ili tuufahamu vyema utamaduni wao na lugha yao wao wanjua vyema zaidi kuliko sisi! Shime jamani tuondokane na mawazo ya kudharau lugha yetu adhimu ya Kiswahili, Hata hivyo nakubali kutokukubaliana kwani kila mmoja ana mawazo na mitazamo yake kuhusu masuala ya kijamii,kiuchumi na kisiasa. Leo hii ukienda Ujerumani unaweza usipate huduma kama hutaongea kijerumani na hapo ni mlangoni na jirani sana na Uingereza.
Tuendeleze mijadala ya aina hii.
Wakatabahu.
Baha.

Chanzo: Wanazuoni yahoogroup

Mama Salma Kikwete aigwe.(Reaction)

Amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yenu Wanazuoni.

Dada Catherine nashukuru kwa mawazo yako ambayo nayeheshimu, ila bado
hujanishawishi. Kwa hiyo RADHI SIOMBI.Pengine tungoje mitazamo ya
wengine. Hata hivyo ingekuwa hoja ni kushurutishana kuombaa radhi,
wallah leo hii ungeshurutishwa wewe kwa kuiona lugha adhimu ya
Kiswahili kuwa dhalili na kuiita 'kilugha'.

Ndugu zangu dhana ya 'vilugha' ni mabano (kwa lugha ya Chambi)
yaliyotengenezwa na wazungu (ambao dada Catherine unajaribu
kuwafagilia) . Lugha ni lugha, Kindengereko ni lugha 'yenye lahaja
zake' Kisukuma ni lugha 'yenye lahaja zake', vivyo hivyo Kiswahili ni
lugha 'yenye lahaja zake' sawa kabisa na Kiingereza ambayo pia ina
lahaja zake.Kwa hiyo ajenda ya 'kilugha' ni dharau tu ya Wazungu
iliyolenga kushusha kujiamini kwa wazalendo. Ikizingatiwa kuwa lugha
ndiyo mlango mkuu wa kuingilia utamaduni wa mtu.Kwa hiyo wazungu
wakauingilia utamaduni wetu, na kwa kweli wakaufanya vibaya na
pengine wanaendelea, wakitutumia sisi kama makuwadi.Je tuendelee
kuingiliwa?

Swali muhimu kuhusu hoja uliyoibua ya 'Lugha ya Kimataifa' ni je
lugha ya Kimataifa huota kama uyoga? Hapana, Historia ya lugha ya
Kiingereza inabainisha kwamba ni juhudi za maksudi (ikiwemo kuziita
lugha za watu wengine vilugha) za wenye lugha hiyo kuieneza, ndizo
zilizoifanya kuwa ya Kimataifa.Ni juhudi kama hizo ninazompongeza
mama Salma kwazo.Lakini nafurahi kwamba dada Catherine umekiri pia
kwa kusema 'wazungu wamekifanya Kiingereza lugha ya Kimataifa'

Pia, dadaangu tafadhali, tafadhali sana, usomi hauwezi kuwa
Kiingereza. Kujua kiingereza usiwe ndio usomi. Haigombi watanzania
kujua Kiingereza. Tatizo hapa ni fahari ambayo watu wanakipa
kiingereza. Huyo Baba wa Taifa hakupigania uhuru ati tu vile alijua
Kiingereza. Hilo pia ni upotoshaji wa Historia, ambayo bahati nzuri,
naifahamu kidogo. Machemba, Mkwawa, Milambo nk, walipambana na
wavamizi bara bara, je hawa walijulia wapi Kiingereza?? . Nyerere
alikuwa mstari wa mbele kuona Kiswahili kinakua, ndiye Nyerere
ninayemfahamu. Alijitahidi kukiweka Kiswahili kwenye ramani ya
dunia.Ni Kiswahili kilichowaunganisha watu ambao leo wanaitwa
Watanzania katika kuukataa ukoloni.

Mwisho, mimi sikatai matumizi ya Kiingereza. Lakini tunakitumia wapi?
Kwa minajili gani? Kwa ulazima upi? Wachina, wajerumani, wajapani, na
nchi kibao za Skandinavia na kwingineko, zinatumia zaidi lugha zao,
zimepungukiwa nini?

Kama Kiswahili si lugha ya Kimataifa, basi ni vema dada Catherine na
wooote wenye mapenzi mema, na tuanze sasa kukifanya kiwe, naam, na
kitakuwa.Kwa kwanzia twaweza kuunga mkono mwelekeo wa Mama Salma.

Ahsante.
Adam, L

--- In wanazuoni@yahoogrou ps.com, "cassianbabygirl"
wrote:
>
> Habari wakeleketwa,
>
> Adam kaka yangu tafadhali acha kupotosha uma nani kakwambia kwamba
> kiswahili ni lugha ya kimataifa?
>
> Hata Mama Salama anapata msaada kwa sababu ni Mke wa rahisi tu na
> bado anachekwa kwa ulimbukeni wake.
>
> Tafadhali note kwamba Hata wazungu wana viruga vyao lkn wamefanya
> Kingeleza kuwa lugha ya mataifa.
>
> Hivi leo hii kama kungekuwa hamna wasome nani angapigania uhuru
> wetu? Lugha ndio imemfanya hata baba wa taifa Marehemu Julius
> Nyerere kutetea Tanzania kwa sababu aliweza kuwasiliana na
> Waingereza.
>
> Kiswahili ni lugha ya Wazaramu , Wandengereko na Wayao Mimi na wewe
> tuna kilugha chetu tunachowasilina tunapokuwa vijijini kwetu.
>
> Hivi ni Kampuni ya nani leo hii itakuwapa kazi kama hujui kingeleza?
>
> Tafadhali naomba uombe radhi kwa kupotosha uma.
>
> Catherine

IChanzo: mjadala wa wanazuoni yahoogroup

Sunday, April 13, 2008

Hekima za wenye Hekima (Wisdom of the Wise)

Do not spoil what you have by desiring what you have not;
remember that what you now have was once among the things only hoped for.

Epicurus

Saturday, April 12, 2008

this is lovely

It's easier to go down a hill than up it but

the view is much better at the top.

Arnold Bennett

Mama Salma Kikwete aigwe.

Tangu alipoingia madarakani, Rais wa awamu ya nne Jakaya Kikwete, mkewe, first Lady Salma amekuwa mstari wa mbele katika harakati mbalimbali. Harakati zake hizo zimehusisha kukaribisha wageni wengi mbali mbali kutoka mataifa ya karibu na mbali.

Mara nyingi, kama si zote, mama Salma amekuwa akitumia Kiswahili katika hotuba zake kwa wageni wake.Hapa ndipo ninapompongeza mama huyu. Mwanzoni wengi wetu tulidhani ni kutokana na yeye kutokuwa bingwa katika lugha ya Kiingereza, lakini nadhani mpaka sasa tumejihakikishia kwamba tulichemka. Mama huyu Mwalimu kitaaluma na kitaalamu, anakijua Kiingereza vizuri kabisa.

Mrengo aliouchukua mama Salma nadhani ni wa maksudi kabisa. Ameamua kuwa Mtanzania anayejivunia Kiswahili. Na kwa hili, amekuwa mfano hata kwa mumewe, Rais wetu JK ambaye naweza kusema anakionea aibu Kiswahili. Mfano mzuri wa kuthibitisha hoja hii, ni pale alipoangushwa na Kibaki na Odinga huko Nairobi, siku si nyingi zilizopita. Baada ya kufanikiwa kuwaweka pamoja ndugu hao wa Kenya, rais Kikwete kwa nafasi yake akiwa kiongozi mkuu wa Umoja wa Afrika, alitoa hotuba yake kwa Kiingereza (Kiongozi wa Kwanza kuhutubia AU kwa Kiswahili alikuwa Chisano wa Msumbiji). Mkapa hakuwa na ujasiri huo!!

Rais wa Tanzania anatoa hotuba kwa Kiingereza katika eneo la Afrika Mashariki, nani abebe bendera ya Kiswahili duniani? Tofauti na kiongozi huyo wa Au, 'faraja' ikaja pale Raila Odinga na Mwai Kibaki walipohutubia kwa Kiswahili. ndipo ninaposema 'walimwangusha JK' hawa Wakenya.

Mwelekeo wa mama Salma hauna budi kuigwa na kuungwa mkono na Viongozi wetu wa Kitanzania. Tunafahamu wanajua Kiingereza vizuri. Lakini wanalo jukumu la kukienzi Kiswahili. Wanalojukumu la Kukieneza na kukitangaza Kiswahili. Wanalo jukumu la kututafutia kazi za ukalimani sisi vijana wa kitanzania kwa wao kuzungumza Kiswahili bila aibu.TUNAWATEGEMEA.WAMECHELEWA SANA.

Ni mara nyingi viongozi wetu wametumia Kiingereza pasipo hata na ulazima wa kufanya hivyo. Inafahamika wazi mathalan, kwamba Rais wetu akienda na ujumbe wake Uingereza, hawezi kuwafanya viongozi wa nchi hiyo wazungumze Kiswahili. Vivyo hivyo akienda Uchina na Japani, watazungumza lugha zao viongozi wa nchini hizo, na ujumbe wa Tanzania utawasiliana na wenyeji wao kupitia Wakalimani na Wafasiri. hiki ndicho alichokianzisha mama Salma. Anakimwaga Kiswahili mtoto wa Kitanzania.Wageni wake wanapata fursa ya kuuonja utamu wa lugha hii adhimu.

HONGERA MAMA SALMA. ENDELEA. KANYAGA TWENDE, HAKUNA KURUDI NYUMA. MJENGA NCHI NI MWANANCHI MWENYEWE.

Pengine wakati umefika kwa viongozi wengine kukienzi Kiswahili kwa kukitumia, hususan katika hotuba zao ndani ya nchi. Bungeni ndiyo kabisaaaa.

Mungu kibariki Kiswahili. Mungu Ibariki Tanzania.

Adam, L

Thursday, April 10, 2008

Congratulations to all Tanzanians

I, as a Tanzanian am proud to have achieved another milestone...The Tanzanian Shilling is now equal to more than 1,200 to 1 US$!!!!
Congratulations to all of us Tanzanians for:
1) Using Chinese toilet paper rather than Rexa or Tanpack...
2) Buying ice cream made in Kenya or South Africa rather than Azam (I agree Ole is not good!!!)
3) Using Omo rather than Foma
4) Eating Heinz baked beans rather than Dabaga or Red gold
5) For using Shoprite as your favourite shopping destination since "expired" South African goods are better than Tanzanian products
6) For using Anchor butter/cheese on your bread rather than ASAS or Serengeti
7) For using Colgate and Close up as they make your teeth brighter rather than Whitedent
8) For drinking Heineken and Red Bull rather than a good old Kili....its a matter of image in it! (Mhabeshi upo hapo?)
9) For drinking St.Anne and Overmeer than Dodoma wine(Mama naihii yako hiyo!)
10) For using Farmer's choice sausages than Beef Vienna from Arusha
11) For using Kangaroo matches than KIBO match .....and the list goes on....
Come on guys wake up....Its time for a change......BE TANZANIAN BUY TANZANIAN.... And a request to the expatriate community...especially South Africans...please change your mind set and help Tanzania grow by supporting local products...
….Hovyooooo!!
Source: Wanazuoni yahoogroup


There might be some light at the end of the tunnel, YES. But we have a long way to go. This photo was taken in Ngorongoro sometime in 2007. PEDP/MMEM had come and gone, jamaa hawa wakabaki kama walivyokuwa.

photo credit: Edward Selasin

Je yaweza kuwa kweli kuwa 'Hata ukioga, mjini huendi?'


Things are not easy to the people of this part of the country. Even when they try to transport their pots so as to open them up for better market, they are constrained by unfriendly transport infrastructure. Some times they end up into huge losses like in this case when the truck overturned. You can imagine on your own as to what happened to their pots.

Indigenous Knowledge base, Utajiri mwingine mkubwa nchini Tanzania


"We are competent in pottery here. We can create in many different forms as you can see: flasks, flower pots, frying pans etc. Our main problem is market. Our pots are of high quality, but do we know where to secure reliable market?" Says, Anna Millinga, of Matema village, Kyela ditrict in Mbeya.

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP