Pekua/search

Wednesday, May 22, 2013

NATAMANI SANA

Natamani sana
Tamaa yangu ni kubwa
Kubwa kuliko niwezavyo sema
Kubwa sana hata siwezi maliza

Tazama watu wa mtwara
Wamepigwa mikwara
Wamepigwa mabomu
Kisa gesi 'yao'

Je ni yao
Yao peke yao
Iwafae wao
Kwa manufaa yao

Ni ya nani?
Je ya kiongozi nani?
Anamiliki nani?
Kwa manufaa ya nani?

Nachelea nisiwe miongoni mwao
Hao wawasemao
Wana wa Mtwara kuwa wamepoka gesi

Nisiwe miongoni mwa wanaolaumu
Eti mataifa ya nje yanaleta chokochoko,
Chokochoko tumeileta sisi
Kwa kutokujua haki za wazawa

Wanayo haki, haki ya kudai pato la gesi,
Wanayo haki ,haki ya kumiliki gesi
Hata kama sheria inasema madini ni ya UMMA,
Wao sio umma au umma wa nani?

Nani atasimama ataonesha usawa katika utajiri wa madini tuliobarikiwa nao
Nani atasimama atasema kuwa eti tumefaidika,,kwa kujengewa shule? Vyoo?
 Kwani TOFARI moja la DHAHABU lajenga VYOO, SHULE, ZAHANATI NGAPI?
Twahitaji MATOFARI mangapi ya TANZANITE ili tujenge barabara?

Wanayo haki,
Ya kutaka kuona namna watakavyofaidika,
Sio kuwapa ahadi
Zile za kwenye majukwaa.

Ifike mahali watu waoneshwe
Wapate kushika,
Hata Tomaso alikataa
Mpaka akatomasa

Vikionekana
Havibishiwi
Vikishikwa
Havikataliwi.

Pengine ni namna tu
Ya walivyodai
Wafanyeje
Kama mahakama ni sehemu ya dola

Wanayo kumbukumbu
Walimu walivyokomeshwa kugoma
Maana mahakama iligoma
Kuwaacha walimu wagome.

Wafanyeje,
WANA wa SIASA si wana WAO tena
Maana wao ni TAIFA teule
Lisiloguswa?

Wana wa SIASA,
Wana HISA
Wanafanya VISA
Utajiri waufaidi wao

Hawakuwa na namna nyingine
Pole wahanga wote
Hamtakwenda bure
Maana mfumo umewapoteza

Guebuza zamani alisema,,if we must die, let us die not like hogs
Hamjafa bure,
Mmefia 'a good cause',
Mungu awape subira, enyi wana wa MTWARA
Itapita hii MIKWARA,
MTASIKIWA.

Tamaa yangu ni kubwa
Kuona mali zetu twazifaidi
Sio kama KIWIRA COAL MINE
Mgodi umefungwa, Kisa ni nini? Waulize wana wa SIASA.

NATAMANI SANA,

WOTE KWA UMOJA TUGOME, TUDAI DHAHABU YETU, TWIGA WETU, NYATI WETU, FALU WETU, TANZANITE YETU, UTAIFA WETU,,,,NA MWISHO UTU WETU,,,


natamani sana,,,,

Tuesday, May 7, 2013

NANI AFANYE NINI?

Bibi yangu miaka ishirini iliyopita aliniambia maneno ambayo sijapata kuyasahau. Nilikuwa nimefadhaika sana ndipo katika mfadhaiko huo nikapata kutamka kitu ambacho kiliamsha hekima ya Marehemu bibi. Aliniambia 'ukiwa na furaha mwanangu (alizoea kuniita mwanae) usiahidi kitu, ukiwa na huzuni usitamke neno lolote na ukiwa na njaa usiahidi kitu'. Nimejitahidi sana kuishi katika hekima hii ingawa kuna muda huwa napotea maana ndio ubinadamu.
Nimeikumbuka hekima hii muda huu baada ya kusikia maana ilitangazwa kwenye redio na kusoma kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu mlipuko wa bomu (ingawa kuna baadhi ya TV zinaripoti kuwa kitu kinachohisiwa kuwa bomu! iwe vyovyote) uliotokea Arusha! Ni muendelezo tu wa yale yaliyotokea siku za nyuma, zilianza kama cheche, sasa zinakuwa si cheche tena! Nilitaraji mtu mmoja angezizima cheche hizi kwani moto hufa kwa kukosa kuni, lakini haijawa hivyo, bali nguvu nyingi zimeelekezwa kuzikataa cheche ambazo zinaongezeka.
Ndipo nikajiuliza niseme nini wakati huu wa fadhaa maana nachelea sana kumlaumu mtu, sasa nifanye nini? Je nikae kimya? Mpaka lini? ndipo nikasema nami niseme japo humu tu. Kwamba nitasikika sijui maana mimi ni mtu mdogo sana, tena sifahamiki kwa yoyote, laiti ningekuwepo mjengoni ningepaza sauti na kutunisha msuri pengine nikiunga mkono hoja,,,maana pasipo hivyo nitatukanwa nami sipendi matusi,,after all its about how much i make in the evening after a single sitting,,hadi raha kukaa tu hela,,,laiti wote tungekaa na kupata hela ingekuwa njema sana,,mmmh nisitoke kwenye hoja yangu ya msingi may be just may be siku moja nitasema umuhimu wa kukaa na kupata pesa,,maana iliandikwa zamani sana ,,KAENI NDANI YANGU,,,,,
Najiuliza nani afanye nini ndio swali langu. Ni kweli tumetikiswa na bomu, ni kweli Padri aliuwawa Zanzibar, je ni kweli vyombo vyetu TUKUKA havijaweza chunguza na kusokotoa nani kahusika? Je tumeshindwa kuwabaini hawa wabaya wanaotugawa sasa? Kuna udhaifu gani huo kupelekea kuwaomba FBI waje kwetu kuchunguza? Je wanachunguza hayo tu au na udhaifu wetu mwingine? Mbona tumeweza kwenda DRC na JESHI LETU TUKUKA? Tumeanguka wapi mpaka kuwaomba hawa FBI? Je yalipotokea mabomu kwenye MBIO za marathoni walituomba? ooh sorry they are better than us,,Je wataishia tu kuchungua bomu? Twahitaji sana kujua nani afanye nini wakati gani,,je si mwenye msiba aliaye sana kuliko waliokuja kuomboleza? Haya maadamu hatujiamini tena nachelea kusema hawa jamaa hawatatuacha mpaka wametuchunga oooh wametuchunguza na kutujua sana zaidi ya tujijuavyo,,mwisho wa siku tutawaomba wawe sungusungu wetu na ndipo tutawatumikia,,,,

Thursday, May 2, 2013

Hoja si meno ya Kinana tunaongelea meno ya TEMBO



Hoja si meno ya Kinana tunaongelea ya TEMBO


“Hoja ya Mzee Kinana hapa inakubalika kimantiki;
'Kampuni ni yangu, kila kitu ni changu ila meno si yangu'

NI KWELI MENO SI YAKE NI YA TEMBO! Lakini sasa huko kwenye kampuni yake huko yamefikaje? Na faida itokanayo na kazi inayofanywa na kampuni yake haiji kwake? Na hata mamlaka zinazopaswa kukagua meli si vya serikali ya chama anachokiongoza? Wanaposema serikali ya CCM in impotent, kwanini asikubali tu?” Fuatilia mjadala huu kwenye facebook http://www.facebook.com/photo.php?fbid=10201162411003067&set=a.1455905638322.64825.1253767086&type=1&theater&notif_t=photo_comment

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP