Pekua/search

Friday, May 30, 2008

MJADALA WA ADVANCED DIPLOMA VS HIGHER DIPLOMA

AMANI IWE NANYI WANAZUONI JADIDI.
NDUGU BAKARIUMEFANYA VEMA KUANZISHA MJADALA HUU.

MFUMO WA ELIMU NCHINI UTAELEWEKA NA KUWA NA MAANA PALE TU SERA ZITAKAPOTUNGWA NA WANANCHI ( KWA NJIA SHIRIKISHI). HIVI SASA TUTAENDELEA KUTUMIKIA MIUNGU TUSIOIJUA, KWANI SERA ZETU NYINGI ZINATUNGWA NA 'WAGENI'.MUNGAI ALIWEZA KULALA NA KUAMKA, HIKI KIKAWA, KILE NA KILE VIKAFUTWA. MSOLA VIVYO, HATA KABLA HAJALALA, ADV.DIP IKAWA IMEFUTWA NA HAYA DIPULOMA INAKUWA.MAGHEMBE KAJA NA YAKE, TENA KWA KASI KULIKO KIPANGA,ETI KIINGEREZA IWE LUGHA YA KUFUNDISHIA KUTOKA MSINGI HADI VYOO VIKUUBWA.TOBA! !! WALIMU TUNAOPATA SHIDA KUFUNDISHA KWA KISWAHILI, TUTAWEZA KUFUNDISHA VIZURI ZAIDI KWA KIINGLISHI, MUNGU WANGU!! HIVI HAWA WADHEE WANATUMIA NINI KUFIKIRI? AU VISIGINO NA SIO UBONGO!!!TUNATUMIKIA MIUNGU TUSIOIJUA NDUGU ZANGU. HAYA MAAMUZI YA MTU MMOJA KUFUMBA NA KUFUMBUA YATAENDELEA KUTULIZA NA KUTUMALIZA. LAZIMA UWEPO MFUMO WA KUSHIRIKISHA WADAU WENGI NA KUZINGATIA MAWAZO NA MITAZAMO ANUAI YA WADAU HAO. HUU MWENDO WA SASA WA WANASIASA KUFANYA KILA KITU NI BALAAA TUPU.NCHI WALA KWA NIABA YETU, NA KUFIKIRI WAFIKIRI KWA NIABA YETU???

JAMANI, TUMENENA SANA, NA ADA YA MJA KUNENA, MUUNGWANA KUTENDA. SASA NATWENDE MITAANI.NAPENDEKEZA , TUSIWE WAPOLE KWA MASUALA YA MUSTAKABALI WA TAIFA LETU.JAPO ULINGO WETU HUU SI RASMI, TUNAWEZA KUJIPANGA KUHAMASISHA MAANDAMANO KATIKA TAASISI ZA ELIMU, WALAU YA JUU, TWENDE MTAANI.TUFANYE MAANDAMANO YA AMANI.DUNIA ISIKIE JAMANI. KWA KWANZIA NAPENDEKEZA MASUALA HAYA MAWILI.TUDAI SERIKALI ITOE MAELEZO YANAYOELEWEKA KUHUSU KAULI ZAKE JUU YA ADVANCED DIPLOMA NA HILI LA KUFUTA KISWAHILI USWAHILI!!!! JAMANI SI DHAMBI. NCHI NI YETU, ALAH!NA SISI NDIYO WANA WA NCHI WENYEWE. TUNAPASWA KUJIRIDHISHA PASIPO SHAKA KUWA MAAMUZI YANAYOFANYWA NA SERIKALI YANAKUWA NA TIJA KWETU NA VIZAZI VIJAVYO, LA SIVYO WANAZUONI TUDAI, TUDAI, TUDAI NA KUDAI UFAFANUZI NA TUSHAURI NA KUSHINIKIZA NJIA MBADALA.NAWASILISHA.
ADAM
Arusha.

--- In wanazuoni@yahoogrou ps.com, "Kiula Kiula" wrote:>>

Amani kwenu wandugu,> > > >
Ninaomba kukosolewa kama nitakuwa nje ya mstari. Advance Diploma ipo juu> kuliko Higher Diploma. Kwa mujibu wa mdau mmoja kutoka NACTE ni kwamba> baada ya kuiphase out Advance Diploma nafasi yake itachukuliwa na Higher> Diploma. Ordinary Diploma itabaki kama kawaida. Kwa mujibu wa NACTE> mambo yatakuwa hivi; Unapotoka A- Level au kwingineko na kujipatia> Ordinary Diploma basi utapaswa pia kusoma Higher Diploma (wanasema kwa> muda mfupi ila sijui ni muda gani), hii Higher Diploma ndiyo itakayokupa> sifa ya kusoma Bachelor Degree.> > > > Asubuhi adhimu.> >

From: wanazuoni@yahoogrou ps.com [mailto:wanazuoni@yahoogrou ps.com] On> Behalf Of BAKARI ISSA> Sent: Monday, May 26, 2008 5:30 PM> To: ethinktanktz@ yahoogroups. com; techtz@yahoogroups. com;> wanazuoni@yahoogrou ps.com> Subject: [wanazuoni]

ADVANCED DIPLOMA Vs HIGHER DIPLOMA COURSES> > > >

habari za kazi na harakati za kulihudumia taifa kwa ujumla> > Naombeni nitumie muda wenu kidogo kulijadili swala hili ili kichwa> changu kipate utulivu kidogo> > "Juzi nliskia kuwa mh. waziri wa elimu ametangaza kwamba wale> waliotayari ndani ya mchakato wa advanced diploma wao watatambulika na> wale wanaoaply sasa wasifanye application for advanced diploma kwani> hazitotambulika kwao"> > ila pia kuna mchakato wa higher diploma ulio vichwani mwetu ambao ndio> utakao replace advanced diploma sasa ninachohitaji kujua ni kama> yafuatayo> > 1: Vyuo karibu vyote vilivyokuwa vinatoa Advanced Diploma naona sasa> vinaendelea kutoa applications for the new intake 2008/09 based on> advanced diploma sasa sijui baadae itakuwaje> > 2: ni vyuo gani vinavyotoa higher diploma? maana nimejaribu> kufuatilia kwa uwezo wangu bila mafanikio> > 3: Je mitaala iliyokuwa ikitumika kwenye advanced diploma ndio> hiyohiyo itakayotumika kwenye higher diploma?> > 4: Vipi system ya elimu ikoje? maana wakati wa mheshimiwa mungai> mambo yalichange kabisa sisi tukiwa kama mfano nikiwa form six 2005> tukalazimika kufanya mtihani mwezi wa tatu badala ya mwezi wa tano, na> mifano mingi iko wazi kwa wanaofuatilia sasa kuna higher diploma Vs> Advanced diploma naomba ufafanuzi zaidi wenye kina na mashiko nadhani> hapa ndio kwenye solution> > > >
BAKARI ISSA> > 3rd Year Student > >
ADvanced Diploma in Computer Science> > Institute of Finance Management (IFM)> > +255 756 876534> > P.O.BOX 77094> > DSM

Chanzo: wanazuoni yahoogroups

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP