Pekua/search

Saturday, October 25, 2008

MWISHO/MWANZO WA AFRIKA!!!!!!!!!


AT CAPE POINT. NILICHOJIFUNZA NI JINSI WENZETU WALIVYOFANYA BIDII KUTENGENEZA KIVUTIO HIKI. TUNAVYOVINGI VYA KUSISIMUA, LAKINI MH! HAVIJATENGENEZWA VYA KUTOSHA.
PILI NILIMSIKIA JAMAA MMOJA - alipokuwa akipanda kuelekea mwisho, au mwanzo wa afrika, ukipenda, akataja KILIMANJARO!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! zis is Kilimanjaro!!! mie bichwaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!NIKIJUA MSHIKAJI ANA HAMU YA KUFIKA K'NJARO (karibu kabisa na katikakati ya Afrika 'ARUSHA Raundi abauti, pale karibu na 'NAZI' hoteli'. Lakini mara kizunguzungu kikazinga kichwani!!!!!!???????

KUTOKA CAPE POINT



Baadhi ya wana AZAKi waliohudhuria Mafunzo ya muda mfupi yaUchambuzi na Ushawishi wa Bajeti Cape Town, Afrika Kusini walipotembelea Ncha ya Afrika huko RASI YA TUMAINI JEMA.Kutoka kushoto ni Rajab Kondo,Elizabeth Missokia wa HakiElimu na Adam Lingson wa Hakikazi Catalyst

Tuesday, October 7, 2008

WENYE MOYO WANAPOJENGA NCHI WASISAHAU KUWANG'OA MENO WALA NCHI

TAIFA HUJENGWA NA WENYE MOYO.
NA HULIWA NA WENYE MENO.
WENYE MOYO WAKIIJENGA NCHI HUKU
WENYE MENO WAKIACHWA KUTANUA MAJIANI
WAJENGAO NCHI WAFANYAKAZI BURE.
WANAKESHA BURE!!!
LAZIMA WENYE MENO WADHIBITIWE.

MOYO KABLA YA SILAHA,
LAKINI SI VITA AU MOYO BILA SILAHA.
"Octavius Kisinda" Add sender to Contacts
To:
wanazuoni@yahoogroups.com
Kamaradi Lingson,

Nimekupata na kukusikia vilivyo. Kinachofuata hapo ni kuchukua hatua mahsusi ili kufikia malengo.

Mchana mwema

The Millenium Court No. 20
8 Cottam Avenue
BRADFORD, Western Yorkshire
BD7 2BT
Mobile: +44 7501 871 805 , +255 754 470 321


'Quid Non Deo Juvante (With God Everything is Possible).'
----- Original Message ----From: lingson adam To: wanazuoni@yahoogrou ps.comSent: Tuesday, October 7, 2008 9:02:37 AMSubject: [wanazuoni] Tanzania itajengwa na wenye moyo SAWA; WENYE MENO JE???
AMANI KWENU WANAZUONI

Hongera pia nakupeni ninyi nyote ambao japo mko mjini mnajisikia kuguswa na kusukumwa kufanya kitu juu ya maisha ya huko kijijini.

Kamaradi Octavius, HAKIKA TANZANIA IMEKUWA IKIJENGWA NA WENYE MOYO. IMEFIKA HAPA (hata kama inachechemea, iko hoi, mahututi au taabani) KUTOKANA NA JASHO LA WENYE MOYO.

KIFUATACHO KWENYE HICHO NA AMBACHO NINADHANI NDIYO WAJIBU WETU MKUBWA KWA SASA NI KUHAKIKISHA TUNAKASIRIKA NA KUJAZIBIKA NA KUWAJAZIBISHA WENZETU ILI KWA PAMOJA TUWANG'OE MENO WALIOKUWA NAYO, AMBAYO KWAYO WANAKULA NCHINI INAYOJENGWA NA WENYE MOYO. AMBAYO KWAYO WANAKULA MATUNDA YOOOOTE YA UHURU BILA KUSAZA, HUKU KINA YAKHE WAKIACHWA KUAMBULIA MAJANI YA UHURU YALIYOPUKUTIKA HAPA NA PALE.

NAWASILISHA
ADAM, L
BOX 16335
ARUSHA, TANZANIA

lingsadam@yahoo. co.uk
www.upolesana. blogspot. com --- On Mon, 6/10/08, Octavius Kisinda wrote:
From: Octavius Kisinda Subject: [wanazuoni] Tanzania itajengwa na wenye moyoTo: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Monday, 6 October, 2008, 10:08 PM
Mpendwa Anastazia,

Nimefurahi na kufarijika kwa jinsi ambavyo umekuwa mmoja kati ya wanazuoni wachane na Watanzania wachache walioweza kujitoa kwa hali na mali kuleta mabadiliko kwa makundi yaliyo pembezoni. Hakika unapaswa kupongezwa na kujifunza toka kwako.

Kwa kuwa mchango wako ni bayana hasa kwetu ambao tumewahi kushi vijini (Usandawe, Kondoa mkoani Dom kwa miaka 5), changamoto ninayoipata hapo ni jinsi ya kuwashauri na kuwashawishi vijana wanaomaliza elimu ya juu kujitolea kulifanya hilo walau kwa mwaka hata mmoja kabla ya kurudi mjini. Kinachonisikitisha ni jinsi ambavyo 'white colour jobs and material accumulation' vinavyoonekana kama ndo elimu kwa sasa. Nadhani tunahitaji kufanya mapinduzi katika eneo hilo na tuone kuwa utumishi uliotukuka wa kujitoa kwa moyo kwa maslahi ya wengi ndo kipaumbele.

Hakika ninayakumbuka kwa dhati maisha yangu ya kijijini kusikokuwa na umeme, barabara ya vumbi na kulala njiani wakati wa mvua ni kitu cha kawaida kabisa, kuendesha pikipiki na kuanguka ni sehemu ya maisha, mawasiliano ni radio simu ya upepo (radio koo) pekee na basi ni mara tatu tu kwa wiki siku nyingine kuifika Dom mjini inakubidi kupanda magari ya mizigo. Ukiwa ndo msomi pekee kwenye tarafa nzima mchango wako unaonekana kwa haraka kulikoni ukiwa Dar kwenye wasomi wengi na wengine wanaotafuta kazi.

Ninafikiria kurudi huko kwa ajili ya utafiti wangu lakini pia kuwatia moyo ndugu zangu kuwa inawezekana. Changamoto niliyonayo ni kuhakikisha kuwa ama ninarudi tena huko au ninahamashisha vijana wengie waende wakapate uzoefu wa Watanzania. Hakika maisha ya elimu, ujuzi na uzoefu usiogusa maisha ya watu hauwezi kuwa ni chachu sahihi ya kuleta mabadiliko endelevu yanayogusa maisha ya wengi.

Kinachonifurahisha ni kuona kuwa kuna Wanazuoni wengi wanaogusa maisha ya watu kwa namna moja au nyingine na hasa walio vijijini. Nikianza kuwataja hapa sitamaliza, bali ninawapongeza kwa utumishi wao ulotumika. Nawatakia mafanikio katika yote yaliyo mbele yenu.

Mungu ibariki Tanzania,
Mungu wabariki wale wote wanaojitoa kwa dhati kwa ajili ya wengi.

Wenu,

KISINDA, Octavius A.
The Millenium Court No. 20
8 Cottam Avenue
BRADFORD, Western Yorkshire
BD7 2BT
Mobile: +44 7501 871 805 , +255 754 470 321


'Quid Non Deo Juvante (With God Everything is Possible).'
----- Original Message ----From: Mbogela Jackson To: wanazuoni@yahoogrou ps.comSent: Monday, October 6, 2008 2:49:07 PMSubject: [wanazuoni] Hongera Annastazia
Hongera Anastazia kwa kazi nzuri Mufindi, Umetoa mchngo wako katika Jamii ya watanzania, tunatahitaji kuwekeza nguvu kidogo sana hapo baadaye kama sasa hivi tutajitolea kluokoa Rasilimali za Taifa zitumike kwa jaili ya walio wengi. Nimeipenda kazi yako Mufindi, Hongera sana. Jackson Mbogela Haarweg 95 – 3166709 PT WageningenThe Netherlands
Cell: +316 43 63 73 73
Tz: +255 787 410 315
Sauti ya Nyika PIUMA WEBSITE PIUMA, IKONDA & TANWAT
Change does not roll in on the wheels of inevitability, but comes through continuous struggle.
Martin Luther King, Jr.
To: wanazuoni@yahoogrou ps.comFrom: neemarug@yahoo. comDate: Mon, 6 Oct 2008 02:16:44 -0700Subject: Re: [wanazuoni] HAPPY BIRTHDAY !
Hongera sana Chambi, u mean a lot to us thatʼs why tunakuombea uongezeke si miaka tu bali ujuzi na maarifa. Keep in mind that the ladder of success is not crowded at the top so keep it up!
HAPPY BIRTHDAY CHAMBI, Bravo

Annastazia Rugaba
Interim Manager-Media Unit
Haki Elimu

NB: Pia nitumie fursa hii kuwasalimia wanazuoni na kuwajulisha kuwa mimi ambaye ndiye katibu wa mtandao huu nimerejea Dar es Salaam toka Mafinga-Mufindi- Iringa-Tanzania nilikokuwa tangu December mwaka jana! nimekuwa na miezi kumi ya maisha magumu kiasi ila yenye vionjo vilivyopevuka. nilikuwa huko nikisimamia Project ya Ku support 200 Orphans & vulnerable children kwa kuwapatia misaada mbalimbali pamoja na vocational training in Electrical Installation, welding and fabrication, masonry and brick laying, Tailoring, Carpentry, food processing and Preservation, chalk making, batik tie & dye, and soap making. Haikuwa kazi rahisi kukaa na vijana 200 wenye matatizo kibao: waathirika wa ukimwi, waliobobea katika biashara hatarishi, wenye matatizo ya akili, wenye msongo na tabia tata kutokana na kupotelewa wazazi, kunyanyaswa na ugumu wa maisha, wahanga wa ubakwaji, wasiojua kusoma wala kuandika, nk. Kuwasimamia na pia kufanya tasks za Manager, Muhasibu, karani, matron, mshauri, mwalimu, afisa na mratibu wa mradi, n.k yote hayo yamewezekana. Kazi imekwenda vizuri na imesababisha kuongezewa fungu la kutosha kurecruit vijana 100 tena kabla project haijaisha.

Atakaependa taarifa zaidi juu ya
· Namna ya kuishi vijijini kikazi na kumudu maisha(kwa vijana wanaotoka vyuoni na hawana uzoefu wa field)
· Namna ya kuleta changamoto kwa jamii masikini ziweze kuhamasika kimaendeleo
· Kuifanya miradi ya wafadhili iwe shirikishi kwa jamii yaani jamii ijisikie kuimiliki miradi na kuleta uadilifu na uwajibikaji
· Kuwamudu vijana yatima na wanaotoka katika mazingira magumu
· Namna ya kupata products zinazotengenezwa na hawa wajasiriamali wachanga kutokana na kozi tajwa hapo juu(kwani licha ya kuwafundisha pia tumewapa mashine, mitaji, elimu ya ujasiriamali na tumewaweka katika makundi na kuakodia business canters)
· Na mengineyo kuhusiana na project hii anaweza wasiliana name sasa niko Haki Elimu nikikaimu nafasi ya Mwanazuoni mwenzetu ambae kwa moyo mmoja ninampongeza sana kwa kupata nafasi ya masomo nje ya nchi. Ninaiahidi tena jamii, wanazuoni na mwanazuoni Nyanda Shuli kuwa nitafanya kazi kwa bidii na kamwe sito waangusha.

Nawashauri wanazuoni wenye uoga na kukimbia assignments za field hata wanapopata fursa hizo, wanakosea sana. Mimi mwenzao nimekombolewa katika hilo, najivunia uzoefu nilioupata katika kazi hiyo na nina uhakika nimewapiga gap kubwa sana graduates wenzangu wengi ambao walipata fursa hizo na kuzipuuza ati kwa kutaka kubaki mjini.
Ahsanteni jamani

CHANZO:wanazuoni yahoogroups

Saturday, October 4, 2008

RAIS KIKWETE AWAJIBIKE KWA KUAHIRISHA ZIARA MBEYA??

AMANI IWE KWENU WAPENDWA WANAZUONI.

Jana nilichangia hoja za ndugu Maro kuhusu kuahirishwa kwa ziara za Rais mkoani Mbeya. Baada ya hapo nimeendelea kulifuatilia jambo hili na kulitafakari zaidi.Mwanzo nilidhani Mkuu wa Mkoa wa Mbeya John Mwakipesile alikuwa na wajibu wa kueleza ukweli juu ya kuahirishwa kwa ziara ya rais mkoani humo kwani sababu alizozitoa hadharani kwa vyombo vya habari kuwa rais hakwenda mbeya kwa vile kulikuwa na mtihani wa darasa la saba na kwamba ulikuwa mwezi mtukufu hazina mashiko (ippmedia.com/ ipp/nipashe/ 2008/09/19/ 122887 .na http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/17107-kikwete-aahirisha-ziara-ya-mbeya.html.

Sababu hizo hazina mashiko kwa vile kwanza licha ya Mwezi mtukufu wa Ramadhani na mtihani wa darasa la saba rais aliendelea na ziara mahali pengine. MATHALANI ALITEMBELEA MKOA WA MANYARA WAKATI WA MFUNGO HUO HUO ULIODAIWA KUMZUIA KWENDA MBEYA (http://www.ippmedia.com/ipp/radio1/2008/09/10/122313.html).

KUTOKANA NA KUKOSA NGUVU KWA SABABU ZA MKUU WA MKOA WA MBEYA, NADHANI NI SASA WA KUWAJIBIKA NI RAIS MWENYEWE. KWANZA AWAJIBIKE KWA KUWACHUKULIA HATUA WALIOUNDA UZANDIKI NA KUSEMA UWONGO HADHARANI KWAMBA RAIS HAFANYI ZIARA MIKOANI WAKATI WA MWEZI MTUKUFU.WAMEMDHALIL ISHA. AWAADHIBU. LA SIVYO BASI RAIS AELEZE WAZI WAZI NI KWANINI HAKWENDA MBEYA KWA TAREHE ZILIZOPANGWA.

NAWASILISHA.
ADAM, L
BOX 16335
ARUSHA, TANZANIA

http://uk.mc254.mail.yahoo.com/mc/compose?to=lingsadam@yahoo.co.uk
http://www.upolesana.blogspot.com/ --- On Fri, 3/10/08, lingson adam wrote:
From: lingson adam Subject: Re: [wanazuoni] JK KUSAFIRI TENA (NINI TATIZO LA MNETE ???)To: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Friday, 3 October, 2008, 12:53 PM
Ndugu yangu Maro nashukuru kwa majibu yenye kuzalisha maswali mengi zaidi.

Ila utanisamehe kwa vile MOYO WANGU UMEKATAA KUAMINI KWAMBA SERIKALI YA JK IMEJAA HOFU NA IMANI ZA AJABU AJABU HATA VIONGOZI WAKE WAOGOPE KUTEMBELEA MAENEO KADHAA ETI KUHOFIA 'KUDHURIKA.' Pamoja na kwamba umemwita Mwandosya rais wa mkoa wa Mbeya, ni wazi hana majeshi huko. Hicho wanachoogopa hao viongozi wakuu ni kipi ambacho vyombo vyote vya ulinzi na usalama vinashindwa kudhibiti??? KWA HISTORIA NAFAHAMU WATU WAMKOA WA MBEYA NI WATIIFU SANA. NA REKODI ZINAONYESHA KWAMBA JK ALIPATA KURA NYINGI ZAIDI MKOANI MBEYA. HAIINGII AKILINI KWAMBA WATU WA MKOA WA MBEYA WANAWEZA KUWA NA KISASI NA JK SASA, MAANA WANGEKUWA NA HASIRA NAYE BASI WANGEMNYIMA KURA ZAO. LABDA TUSEME YEYE JK NDIYE MWENYE KISASI NAO??? LAKINI KWA LIPI???? naulisaaaaaa! !!!!!!!!! !!!!!

kama kweli viongozi wakuu wa kaya hii wanaogopa kwenda mbeya kwa sababu yoyote ile, BASI WANAOGOPA VIVULI VYAO TU. NA BASI BORA TUKAUSIMIKA MTI, KISIKI AU MLIMA WOWOTE UTUONGOZE KULIKO WALONGOZI WAOGA NAMNA HIYO!!!!!!!!
sitaki kuamini kirahisi

Kaka Maro, na HILI LA SUDI MNETE??????? ????????? ????????? ?????? Naamini ukipata muda utalitolea ufafanuzi.

NAWASILISHA.
ADAM, L
BOX 16335
ARUSHA, TANZANIA

http://uk.mc254.mail.yahoo.com/mc/compose?to=lingsadam@yahoo.co.uk
http://www.upolesana.blogspot.com/ --- On Fri, 3/10/08, Yona Fares Maro wrote:
From: Yona Fares Maro Subject: Re: [wanazuoni] JK KUSAFIRI TENA (NINI TATIZO LA MNETE ???)To: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Friday, 3 October, 2008, 11:19 AM
Ahsante kwa kuuliza nitakujibu kwa ufupi lakini kwanza kuhusu suala hili la mbeya .

Mzozo kuhusu mbeya ulianzia wakati ule wa kumchagua mgombea wa uraisi toka chama cha mapinduzi kulikuwa na makundi kule mbeya walikuwa wanamtaka raisi wao mwandosya , wao walitegemea yeye ndio atapita lakini ndani kwa ndani akachomewa utambi akabwangwa na huo ndio ukawa mwanzo wa hizi choko choko za mpaka leo .

Kama unafuatilia mambo mtu wa kwanza aliyetakiwa kulipia alichofanyiwa Mwandosya wakati wa kampeni zile ni Lowassa wakati fulani alitakiwa awe kwenye safari ya mkoa ule kama waziri mkuu lakini akashindwa kwenda kwa sababu alikuwa amelewa sana alitoka kwenda sherehe ya mtoto wake ile iliyotumia zaidi ya mil 300 , akatumwa juma akukweti akamwakilishe na safari yenyewe ilicheleweshwa mpaka saa 8 ndio alitoka dar kwenda mbeya muda wote huo lowassa alikataa kwenda .

Wakamkosa Lowassa akapatikana akukweti na hata yeye alicheleweshwa kupelekwa hospitali kwa sababu zao tu wenyewe wanazozijua alikaa zaidi ya masaa kadhaa
"If you won't take the personal responsibility to help raise the level of debate on PwaniForums, you do not have much of a case for expecting anyone else to do so on your behalf." --- On Fri, 10/3/08, lingson adam wrote:
From: lingson adam Subject: Re: [wanazuoni] JK KUSAFIRI TENA (NINI TATIZO LA MNETE ???)To: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Friday, October 3, 2008, 7:13 AM
AMANI IWE KWENU

SHUKRANI KWA KUTUHABARISHA NDUGU MARO.
KUHUSU MBEYA:
KUNANI MBEYA HATA RAIS WA NCHI AOGOPE KWENDA???? AU KUNANI MOYONI KWA JK HATA AJIKUTE NAFSI YAKE IKISUTWA???? ? AMA KUNANI AKILINI KWETU KINA SISI WACHAMBUZI TUNAOJARIBU KUENEZA UWEPO WA FITNA,HOFU, MASHAKA, TISHIO LA USALAMA HUKO MBEYA HATA KUJARIBU KUUFANYA MKOA WA MBEYA KUWA NA TASWIRA YA MKOA WA AJABU KIASI KWAMBA RAIS ALIYEPIGIWA KURA NA WANANCHI WA MKOA HUO HUO NA AKASHINDA KWA KISHINDO ANAOGOPE KUFANYA ZIARA???

ZAIDI YA YOTE TIJA YA ZIARA YA RAIS KWENYE MKOA WOWOTE NI IPI???WATANZANIA TUCHAPE KAZI. RAIS MAKINI NA MAHIRI ANAWEZA KUSIMAMIA MAENDELEO YA NCHI VIZURI KABISA KUTOKEA IKULU YAKE NA KUPITIA MIFUMO YA KIUONGOZI NA KIUTAWALA ILIYOPO. SI LAZIMA AENDE KILA MAHALI KUUZA SURA YAKE. IWAPO TUTAKAZANIA KUAMINI NA KUWAAMINISHA WANANCHI WENZETU KWAMBA MATATIZO YAO HAYATAWEZA KUONDOSHWA MPAKA TU-RUB SHOULDERS NA RAIS, BASI TUMO HATARINI.

Mwisho Kamaradi Maro, sidhani kama shambulizi ulilofanya kwa Mnete kuwa ni la haki. Je hatangazi kwa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo??Pengine mwenzetu utwambie UNAJUAJE KIWANGO CHA TAALUMA YA KILA MTANZANIA, wewe ni nani hasa kaka?? NA PIA TUTAABUDU MADIGRII YA KARATASI HATA LINI???KOSA LA MNETE LIKO WAPI KWA YEYE KWENDA KWENYE ZIARA YA RAIS?? NA UNATHIBITISHAJE IWAPO ANAYEMLIPIA NI JK AMA SERIKALI NA SI CHOMBO CHAKE (ITV)?? KUONGOZANA NA RAIS KUNA SHIDA GANI? JE WAWEZA KUTOA USHAHIDI UBAONI KUTHIBITISHA UTENDAJI ULIOCHINI YA KIWANGO WA SUDI MNETE NA KWAMBA UMETOKANA NA KIWANGO CHAKE USICHOKIELEWA CHA KITAALUMA NA KITAALAMU?JE HUDHANI KAMA UMETUMIA JUKWAA HILI KUMDHALILISHA MNETE?? pima mwenyewe!!!Chukua hatua.

NAWASILISHA.
ADAM, L
BOX 16335
ARUSHA, TANZANIA

http://uk.mc254.mail.yahoo.com/mc/compose?to=lingsadam@yahoo.co.uk
http://www.upolesana.blogspot.com/ --- On Fri, 3/10/08, Misha wrote:
From: Misha Subject: Re: [wanazuoni] JK KUSAFIRI TENATo: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Friday, 3 October, 2008, 9:40 AM
Heeeeeeeeeeeeeeee, ushasahau kuwa, huko huwa anaenda kutafuta wadau wa maendeleo kwa taifa letu kama vile wawekezaji

Na je umeshasahau kuwa akirudi atakuwa ameahidiwa, kwamba Tanzania itapewa msaada wa kiasi fulani cha fedha.

Jamani hivi umesahau kuwa ombaomba si lazima kujipanga barabarani na kikopo cha bati, huku ukisema saidia baba saidia mamaaaaaaaaaaaaaaa.

Inawezekana kuna kuwa ombaomba ya kiutaalamu zaidiiiiiii! !!! jamani subiri atakuja kaahidiwa mabilioni ya pesa, na yeye amekubaliana na mambo fulani ya kibinafsishaji
Sasa sijui hiyo itakuwa ni WIN WIN situation ama WIN LOSE situation??? ?
MAZUNGUMZO YATAKUWA HIVI

Jei Kei: Saidia baba

Wadau wa maendeleo ya Tanzania nchi za nje: Nikusaidia nini mbona una rasilimali kibao

Jei kei: Kuzifaidi inahitaji kufikiri baba tena na investment ya hali ya juu nasi hatuna.

Wadau wa maendeleo ya Tanzania nchi za nje: http://uk.mc254.mail.yahoo.com/mc/compose?to=&?@@@$$$$*******&&&&&&!!!^^^????!! !!

Jei kei: Tafadhali njoo uwekeze nami nipatiemo kidogo, eeee baba tehe tehe. PLEASE

Wadau wa maendeleo ya Tanzania nchi za nje: Dont woree, i will help you, Dont distabu your mind. THINKING IS TOO HARD, I WILL THINK FOR YOU

Jei Kei: seikyu vere muchi
Alamsiki--- On Thu, 10/2/08, Yona Fares Maro wrote:
From: Yona Fares Maro Subject: [wanazuoni] JK KUSAFIRI TENATo: "techtz alphonse" Cc: wanazuoni@yahoogrou ps.comDate: Thursday, October 2, 2008, 6:40 AM
Raisi jakaya mrisho kikwete anatarajiwa kusafiri tena kuelekea nchi za amerika ya kusini kuanzia wiki mbili zijazo , anatarajiwa kwenda brazil , cuba pamoja na Venezuela , anazidi kutuka viunzi tena kuhusu safari yake ya mkoa wa mbeya ambayo inasemekana alitakiwa aifanye baada ya mwezi mtukufu .

Ziara nyingi za raisi zimekuwa zinasindikizwa na misafara mirefu ambayo haina umuhimu wowote katika safari hizo pamoja na waandishi wa habari ambao hawakidhi fani hiyo ya uandishi kama sudi mnete wa ITV ambaye elimu yake ya uandishi wa habari haieleweki vizuri nab ado anaongozana katika misafara hii ya raisi .

Sasa ni wakati kwa wananchi wa Tanzania haswa wadau wa habari kuanza kuhoji kuhusu safari hizi haswa gharama zake na faida zake kwa taifa , miaka michache iliyopita waziri mkuu mstaafu aliwahi kusafiri kwenda ulaya aliporudi watu walilalamika sana kuhusu safari hiyo na garama zake .

Basi jambo hili pia lifanywe kwa raisi wetu na wale wote anaoongozana nao katika misafara hii watanzania wajue kinachoendelea ni nini haswa

SOURCE: WANAZUONI YAHOOGROUP

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP