Pekua/search

Tuesday, January 27, 2009

KUBATILISHA LESENI ZA WAGANGA: WANASIASA WETU WATAACHA KWENDA BAGAMOYO, PEMBA, SUMBAWANGA N.K


Enyi wanazuoni weledi,

mwenzenu nauliza tu;
Je ndiyo kusema hatuwaoni tena viongozi wetu wakikimbizana Bagamoyo nyakati za uchaguzi?
Je watavua mapete (yanayohusishwa na imani za kiganga) makubwa makubwa vidoleni mwao?
Je mfumko wa biashara ya vichanga na viungo vya binadamu hospitalini ukitokea, serikali itapiga marufuku utabibu wa kimagharibi?
Je wametumwa na nani na wanataka kumfurahisha nani?
Je tupumue sasa, kwamba maalbino hawauawi tena? Is it an easy n cheap solution to the problem?
Je hatujidhalilishi kama watanzania wenye historia yetu
Je hicho kitengo cha muhimbili kinawathibitisha kwa viwango alivyoweka nani?
Je indigenous knowledge base yetu lazima ifanane nay a kimagharibi?
Kwanini wasishirikishwe? Mbona ni kama wameonyesha ushirikiano mahali pengine?
Motto wa mkulima Pinda anasema kama waganga wa jadi wangekuwa wa kweli na wa uhakika basi magonjwa yangepungua, je hospitali nazozipigwe marufuku? Maana zipo na magonjwa yapo kede kede,
Kwanini mtoto wa mkulima hasemi chochote kuhusu kutotungwa kwa kanuni za kutekeleza sheria ya tiba asilia ya mwaka 2002?

Tumefedheheshwa na dhalilishwa sana na tabia ya wenzetu kuwawinda wenzetu (albino) kama wanyama pori , lakini majibu rahisi rahisi kama hili la serikali, sijui kama yatatusaidia sana . Ningedhani kuwasajili kungesaidia sana kuwajua kuliko vinginevyo!!!

Je baada ya kupiga marufku unafuata msako wa kuwajua iwapo wanaendelea? Kama ndiyo, serikali imeshindwaje kuwakamata waganga wanaowaua au kuchochea mauaji ya albino? NAULISA TU

rejea:http://thecitizen.co.tz/newe.php?id=10084
Ilitolewa wanazuoni yahoo groups

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP