Pekua/search

Wednesday, April 24, 2013

Chanzo cha Ubovu wa Elimu ya siku hizi ni ‘Ubora' wa Elimu ya Zamani?



Chanzo cha Ubovu wa Elimu ya siku hizi ni  ‘Ubora' wa Elimu ya Zamani?

Picha imebebwa kutoka http://philosophyforchange.wordpress.com/2010/09/29/unlearning-in-crisis-and-change/
Linapokuja suala la ubovu wa elimu, sio kuporomoka kwa kiwango cha ubora wa elimu nchini Tanzania hapana shaka utasikia elimu ya zamani ilikuwa bora elimu ya siku hizi hamna kitu! Hata suala ;la malezi utasikia watoto wa siku hizi wameharibika. Hii imekaaje? Zamani ni lini? Waliosoma vizuri zamani wako wapi hivi sasa au walikuwa wapi hadi elimu ya siku hizi imekuwa mbaya? Gwankaja anajiuliza kwenye facebook hebu fuatana naye kuitafakari nadharia ya KUYAKIUKA ULIYOJIFUNZA ILI UJIFUNZE MAPYA...

KAMA ELIMU YA 'ZAMANI' ILIKUWA BORA, HII YA SASA MBOFU MBOFU IMEKUJAJE WAKATI WALIOFUNZWA VIZURI NDIYO WAKO KWENYE USUKANI SASA? HIVI WASIMAMIZI WA ELIMU YA SIKU HIZI WALISOMA LINI?- ZAMANI!!!
KAMA MALEZI YA 'ZAMANI' YALIKUWA BORA, HAYA YA SASA YANAKUWAJE MABAYA WAKATI WALIOLELEWA VIZURI NDIYO WAZAZI SASA? WAZAZI NA WALEZI WA SIKU HIZI SI WALIZALIWA NA KULELEWA ZAMANI? Huu mzabibu pori unakujaje? Naulisaaaaaa.....
Nadhani Tukitaka KUINUA UBORA WA ELIMU YETU TUTAZAME KWA MAPANA YAKE TOFAUTI NA HIVI SASA AMBAVYO TUNAPAMBANA KUIREJESHA KUBOVU ILIKOTOKA. Tukubali kuwa kama taifa kuwa mzizi wa matatizo haya ni mrefu....

We need to Unlearn more than learn..au basi We need to Learn to Unlearn so as we can Learn better.





0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP