Pekua/search

Thursday, July 15, 2010

TRIBUTE TO PROF. JWANI MWAIKUSA


Sikumfahamu sana,

Hilo sitajisifu,

Zaidi ya mshairi mahiri,

Kwamba ndio wake wasifu.

Nilisoma kwa makini,

Nilipojua tu kusoma,

Nikajiuliza samoni (summons)!!

Ni ile ya mahakama?

Huyu fighter, alowaza,

Mimi sikulibaini

Alikuwa na maana gani, nikajiuliza mimi



Ulazwe pema msomi

Pumzika kwa amani peponi,

Twalia, twaomboleza.

Nuru yako ya wema

Mwangaza wako wa upendo

Kamwe hautazimika!!

Kwa walokujua na wa mbali

Watakuenzi daima



Nenda ‘Fighter,

Nenda,

Ee mola wetu mwema,

Ulosheheni rehema,

Waloinyang’anya haki,

Ya profesa kuishi,

Wale maharamia,

MUNGU UWASAMEHE,


Prof. Mwaikusa was murdered by unidentified people (armed robbers??????) Tuesday 13th July, at his place in Dar es Salaam.

NA UTUSAMEHE!

3 comments:

John Mwaipopo August 25, 2010 at 9:38 AM  

shairi lake moja linaitwa 'an awful dentist'. halichoshi kusoma na usomapo utabaki kucheka tu na utakapomaliza kucheka utahudhunika baada ya kulitafakari na kupata nini alimaanisha.

Adam August 25, 2010 at 10:46 PM  

Ahsante John.
Tanzania imepoteza shujaa wa aina yake. Tafadhali kama una nakala pepe ya shairi hilo nishirikishe tafadhali. Waweza kulibandika hapa ama nitumie kwa lingsadam@yahoo.co.uk.
Kazi njema.

Anonymous July 16, 2012 at 6:49 AM  

Asante kaka

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP