Pekua/search

Tuesday, February 7, 2012

WANASIASA WANAWATUMIA WASANII KAMA KONDOMU - SINGLE USE ONLY

Mzee Sefu
Mzee Thabit Sefu wa mjini Mbeya amekuwa kwa muda mrefu akitumbuiza  kwenye hadhara mbali mbali mjini mbeya hususan za kisiasa. Ujumbe wa nyimbo zake katika ngoma yake yenye asili ya kingoni almaarufu kama DZOMBE umekuwa ukichoma moyo, kuamsha hisia na kufikirisha. Zaidi sana amekuwa nguvu kubwa ya kuwakusanya watu. Nilipofanya mahojiano naye mwaka 2007 alikuwa hakumbuki umri wake lakini kulingana na matukio anayokumbuka na kuhadithia alikadiriwa kuwa na miaka 80. Mzee Sefu amepitia mikasa mbali mbali ikiwemo kuchimbwa mkwara kwa kutumbuiza kwenye shughuli za VYAMA VYA SIASA VYA UPINZANI. Soma makala HAPA.

Hivi sasa hali ya mzee huyu inaelezwa kuwa mbaya sana (Bonyeza HAPA kufuatilia mjadala kwenye facebook). Si wanasiasa wa CCM ama wa Upinzani wanaomtupia jicho. Kama KONDOMU wamemtumia, wamefanikisha malengo yao, Washamaliza haja zao, WAMEMTUPILIA MBALI. Usanii ni laana nchini? kipaji ni balaa!!! Pole mzee SEFU.


0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP