Pekua/search

Saturday, April 21, 2012

TUNAWEZA HATA KUFUGA FISI - Tunayo maarifa mengi

Tunayo maarifa mengi. Kwanini Hatuendelei kwa kasi zaidi?


Msanii wa ngoma ya asili ya Kisukuma (jina halikupatikana) akionyesha fiisi wakati kikundi chake kilipotumbuiza katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika kijiji cha Chela wilayani Kahama Februari 25, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).


Mjadala kwenye Facebook:


Shununa Isaack kaka adam,asb njema kwanza.huyo jamaa ana kibali chakufuga hujo fisi?au jamaa mambo fulani...

Adam Gwankaja ahsante, na iwe njema sana na kwako dadaangu Shununa Isaack. Hapo sasa kwenye swali lako ndipo tatizo linapoanzia. sheria zetu nyingi ni za kipuuzi sana, maana hazizingatii traditional au ile indigenous knowledge base. Zimeatikwa tu kutoka hukooo ughaibuni. mfano ni Kwanini awe na kibali? Kwani kufuga mbwa twachukua vibali? Usukumani, FISI ni mali aiseee. ha ha ha haaaaaa. Anaweza kuwa mnyama pori au wa kufugwa, upo?? Sikiza sasa wapigania haki za wanyama wenye mrengo wa kimagharibi!!!

Niitiwe Mwansasu Kaka huenda hata siyo fisi, binadamu wana mambo mengi huwawezi!!! Jiulize amempata wapi?

Adam GwankajaNiitiwe Mwansasu, kwani mbwa tunawapata wapi? Hiyo ni indigenous knowldge mwana wane. Usukumani fisi aweza kufugwa bila taabu ujue.

Niitiwe Mwansasu Wenye kwao watanisamehe lkn Dom wanafuga punda ila kwa baadhi ni kitoweo na kuwasaidia kubeba mizigo!! Sasa anawasaidia nini km co mambo fulani....???

Adam Gwankaja ha ha haaaaa dadaangu weye!!!! hata hayo mambo flan ni maarifa, ila ukristo ulipkuja ukatuharibia sana, na tukazidi kuyaficha; tukayaficha yale distructive na constructive kwa pamoja. moja ya matumizi ya fisi huku naambiwa ni USAFIRI!

Shununa Isaack nakubaliana nawewe kaka adam.makatiba yetu sio.watuache tujifugie manyoka,fisi nk.mi ntafuga tembo na jamaa simba.niwaone wezi.pia siku navuna meno yangu ya tembo nisione mtu anasogea.pia kaka wale swala ntafuga kwa wingi kila siku kamoja kanaliwa.upo hapo vyetu bwana

Niitiwe Mwansasu Mpendwa wangu hayo mambo fulani yana faida gani kwetu? Mbona tunazidi kuwa masikini wa kutupwa! Makubwa usafiri wa fisi unakuwaje? Jamani hebu wamkumbuke mungu kwanza ili awasaidie!!!

Adam Gwankaja Ha ha ha haaaa ushaanza fujo zako Shununa Isaack dadaaangu. Tamaduni ni muhimu. majuzi hivi nilikuwa Nepal huko mashariki chini ya Himalayas, nimestaajabu wanafuga tembo ujue. Hana fujo wala nini. Ziko nchi nyingine wanafuga mbogo/nyati ujue.

Adam GwankajaNiitiwe Mwansasu kwa hali iliyomo leo baada ya uharibifu uliofanywa na ukoloni na utamaduni wao, nakubaliana na wewe. Lakini tumekosea sana kudhani kila maarifa asilia ni dhambi. sio kweli. mfano mdogo, wamisionari waliwakataza wazee wetu hata kutumia mitishamba, leo wamerudi na products za miti ile ile (alovera kwa mfano) wanatufundisha kuitumia. So nalitazama suala hili kwa upana namna hiyo. Kwamba yako maarifa yetu yanapotea, na kuzidi kupotea.

Kujiunga na mjadala: bofya HAPA

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP