Pekua/search

Friday, July 20, 2012

Je Wamjua ‘Mtu’ wa Kwanza kuona chanzo cha mto Ruvuma?


Je Wamjua ‘Mtu’ wa Kwanza kuona chanzo cha mto Ruvuma?
Ni leo (Julai 21) katika Historia yetu

Hapo mwaka 1886, Askofu wa Kanisa la Anglikana, Charles Alan Smythies, alikuwa MZUNGU sio mtu wa Kwanza kuona chanzo cha mto RUVUMA. Inaelezwa kuwa Askofu huyu alifika katika chanzo cha mto Lujenda, naodaiwa kuwa chanzo muhimu cha mto Ruvuma.
Inasemekana kwamba wakati askofu huyo alipokiona chanzo hicho, uvumi ulienea miongoni mwa wenyeji kwamba kwa vile chanzo hicho kilikuwa na MASHETANI basi Askofu Smithies angekufa. Hata hivyo askofu huyo hakufa kama ilivyohofiwa.

Vile vile yafaa kukumbushana hapa kwamba Askofu Charles Allan Smithies ndiye alikuwa askofu wa kwanza wa UMCA (University Mission to Central Africa) – ya Anglikana visiwani ZANZIBAR hapo mwaka 1892. Leo hii miaka zaidi ya mia moja, karne nzima…Wanaharakati wanaojiita wa kiislam wanachoma makanisa, ilhali pale mkunazini minara miwili, Msalaba na mwezi) imekaa sambamba kwa ujirani mwema kabisa kwa miaka nenda urudi bila fujo.

 Bishop Charles Allan Smithies succeeded Steere and he became the first bishop of UMCA to be titled Bishop of Zanzibar the commemoration of Bishop Charles went together with the Zanzibar to become a diocese, hence the Diocese of Zanzibar was established 1892.

Kanisa KONGWE lililoko MJI MKONGWE huko TANZANIA VISIWANI

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP