Pekua/search

Friday, July 20, 2012

Janga juu ya Janga: Dharau ya Madereva kwa bodaboda


Dharau ya 'waendesha magari' kwa bodaboda ni janga la kitaifa pia

Tangu ‘mchina’ alipochochea mapinduzi ya kifikra nchini kuhusiana na usafiri, kumekuwa na ajali nyingi zinazosababishwa na usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda hata baadhi ya watu maeifikia hatua ya kuita bodaboda kuwa ni janga la kitaifa.

Sababu nyingi zimeelezwa kuwa chanzo cha ongezeko la ajali hizo ikiwa ni pamoja na kukosekana umakini, kutojali na kutozingatiwa kwa misingi ya usalama barabarani ikiwemo udereva wa kujihami kwa upande wa madereva wa bodaboda ambao wengi wao hawana hata mafunzo ya msingi ya kuendesha vyombo hivyo vya moto.

Lakini iko sababu nyingine ya kuongezeka kwa ajali za bodaboda na ambayo kwa bahati mbaya sana hainyooshewi kidole mara kwa mara. Sababu hiyo ni DHARAU ya kupindukia miongoni mwa waendesha magari dhidi ya bodaboda. Dereva wa gari kwa kujua kuwa vyombo vyao ni madhubuti kuliko boraboda wamekuwa wakiwafanyia fujo bodaboda na mara nyingi kuwaumiza. Ninayo mifano mingi inayoshuhudia hili, lakini  wacha niuseme huu mmoja tu nilioshuhudia siku za karibuni.

Tunafika kituo cha mafuta pale Mlimani City, nashuka kwenye bodaboda kupisha iwekewe mafuta…dereva wa bodaboda ambaye ni Rafiki na jirani yangu anasogeza chombo chake kipate mafuta, mhudumu wa kituo cha mafuta anafanya kile kinachopaswa.

Hilo likiendelea anakuja mwenye gari analisogeza karibu kabisa kwenye pikipiki kisha anafungua mlango kiasi kwamba Rafiki yangu Katale anashindwa hata kutoa mguu. Kila mmoja anashangaa. Bahati nzuri kwa ustaarab mkubwa, dereva wa bodaboda, anahangaika kukinasua chombo chake hasemi hata neno. Mimi naishia kutwanga picha tu na dada aliyekuwa anajaza mafuta kwenye bodaboda anabaki kinywa wazi kwa mastaajabu. Picha hiyo inasema kila kitu.

Pamoja na matatizo mengi yanayohusisha matumizi ya usafiri wa bodaboda ikiwemo ajali na vifo, ni ukweli usiopingika kwamba bodaboda zimesaidia kupunguza matatizo ya usafiri kwa watu wengi hususan wenye kipato cha kati kwenda chini. Pia bodaboda zimesaidia sana kuchochea ari ya kujishughulisha miongoni mwa vijana ambao vinginevyo wangekuwa  vibaka wezi na ama majambazi kabisa. Suala la kupunguza msongamano wa magari barabarani nalo ni moja ya faida za bodaboda.

Ni vema basi tunapohimiza umakini miongoni mwa waendesha bodaboda, tuwasisitizie pia waendesha magari kuwaheshimu watumia bodaboda, maana nao ni watumiaji halali wa barabara. Katika kujilinda madereva wa bodaboda wameanzisha umoja na wamekuwa na nguvu ya ajabu. Ukimfanyia fujo mmoja wanashambulia zaidi ya nyuki au vikosi vya NATO. Hivyo hala hala wandugu usijekuta unaumia kwa kuendekeza dharau

4 comments:

Unknown July 22, 2012 at 4:10 AM  

Adam, im just keen to know where that bodaboda guy got those words down his number plate! purely Luganda!

Thanks

Asifiwe July 22, 2012 at 6:45 AM  

hili ni tatizo,haliishii tu kwenye bodaboda ukipita njia ya bagamoyo or sorry barabara ya bagamoyo waendesha malori hawawajari hata wenye magari madogo, jana jioni tumenusurika kugongwa mimi na jamaa yangu, kisa tuna ka VW afu mshikaji ana FUSO. Hivyo msisitizo uwe wenye magari waheshimu matumizi sahihi ya barabara

Adam July 22, 2012 at 11:49 PM  

Ha ha haaaa Unknown' those words are Bantu. It is a kihaya, I presume. All is for God something like that, or...all belongs to God. the haya shud be related to Luganda

Adam July 22, 2012 at 11:52 PM  

Asifiwe ndugu yangu... nashukuru sana kwa kutupa upana wa suala hili. Hapo DHARAU ndiyo inayotuua. Kila mwenye kidogo hafai anapuuzwa na kunyanyaswa... Walisema wahenga wa kigeni...

Most people are bad..when they are strong they take from the weak.. most good people are weak, they lack strength to be bad.

Msemo mbaya kweli kweli..lakini yawezekana unao ukweli ndani yake.

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP