Pekua/search

Thursday, July 19, 2012

Ningekuwa daktari ningekubaliana na wito wa serikali


Ningekuwa daktari ningekubaliana na wito wa serikali;

  • Ningekubaliana na kauli ya Rais Kikwete..ama ningerudi kazini au ningejiendea huko kwingine.
  • Ningeunga mkono kauli ya waziri mkuu litakalokuwa na liwe
  • Uzalendo hauwezi kuhimizwa na viongozi wasio nao

Nimesoma makala kwenye gazeti la Raia Mwema toleo la jana kwamba madaktari kadhaa wameitikia wito wa serikali kurudisha leseni zao za udaktari kama walivyoagizwa kufanya. Na kwamba zaidi ya madaktari 50 kati ya takribani 400 walio’futwa kazi’ na serikali wanafanya mipango kwenda nchi moja rafiki. La zaidi kwamba nchi kama Namibia, Botswana, Lesotho, Sudan Kusini, Rwanda na Swaziland zinafanya jitihada ya kuwadaka wataalamu hao adhimu na adimu waende wakafanye kazi huko.

Wakati tunapowapongeza madaktari walioitikia wito wa serikali na kurejea kazini kufanya kazi bora liende-liwalo na liwe hata kama huduma hazitaboreshwa, nawiwa pia kuwapongeza hawa wengine walioitikia wito wa serikali kupitia mtendaji wake mkuu yaani Rais Kikwete kuwa waende wanakoweza kupata mazingira bora ya kazi ikiwemo malipo bora zaidi.

Naam, naona wenzetu wameanza kuchukua hatua. Serikali imechukua hatua kwa kuendelea kugoma kutimiza mahitaji ya madaktari nchini na madaktari wengine wamechukua hatua za ama kurejea kazini au kurejesha leseni na kuanza kutafuta maisha kwingineko. Kibarua kinabaki kwa wananchi kina sisi kufanya maamuzi na kuchukua hatua dhidi ya serikali tuliyiweka madarakani ikusanye kodi na kusimamia raslimali tulizojaaliwa nchini na kasha itupatie huduma bora! Sijui tutaendelea kukaa kimya mpaka lini? Oh sorry, kumbe nasi tumefanya maamuzi tayari, yaani kukaa kimya! Safi kabisa.

Nukuu kutoka Gazeti Raia Mwema,
Wapo madaktari 50 tayari wamekwishakuzungumza na Waziri wa Afya katika moja ya nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara ili waende kufanya kazi huko na kwa kweli kuna makubaliano watakwenda huko lakini wakifika wataingizwa katika mfumo wa mafunzo ya kidaktari kwa vitendo (interns). Watakuwa chini ya uangalizi wa madaktari wengine ili hatimaye kuwapa uhalali wa kitaaluma wa kuwa na leseni ya udaktari,” kilieleza chanzo chetu cha habari.
Kusoma habari kamili Madaktari warejesha leseni bonyeza kiunganishi kifuatacho

1 comments:

Asifiwe July 20, 2012 at 6:08 AM  

wananchi tumegoma kwa kuwa hatujui kuwa sisi ndio wenye mamalaka kubwa kushinda hao tuliowakabidhi hayo madaraka,,

watu ambao hawana priority tumewafanya wawe viongozi wetu,,twataraji nini? zaidi ya liwalo na liwe? zaidi ya kusema nendeni mnakoona kunawafaa. Najiuliza yeye Kikwete anawahitaji hawa madaktari? wa nini wakati anaye wake peke yake? wa nini hawa wakati yeye anauhakika wa tiba bure mpaka Mungu amchukue? wa nini yeye wakati wanae wamo kwenye mfumo nao wanatibiwa bure, wanakula IKULU? Wa nini kwao? liwalo na liwe

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP