Pekua/search

Monday, July 16, 2012

Moral obligations si kwa madaktari tu


Moral obligations si kwa madaktari tu
  • Serikali iwe mstari wapamoja
  • Viongozi wa sekta ya afya waonyeshe mfano
  • Madaktari hawaruhusiwi kugoma lakini wana ukomo wa uvumilivu kama binadamu wengine
Dr Marina Njelekela CEO wa Muhimbili.
 Jana katika kipindi maalum kilichorushwa jana (16/7/2012) usiku na televisheni ya taifa TBC kuhusu mgomo wa madaktari mambo kadhaa yamenigusa:

Kwanza, Mtangazaji Shaaban Kisu, ameendesha kipindi kile vizuri, ameuliza maswali ya mazuri kwa ujumla kiasi kwamba amenifanya nione fahari ya TBC kuwa chombo cha Umma. Nampongeza kaka Shaaban kwa kutimiza Professional Obligations vizuri pasipo kukiCCM au KukiSerikali kipindi hicho kama wafanyavyo wengine.

Jambo la Pili nimeguswa na jinsi wasomi wan chi hii; CEO wa MOI Prof Laurence Mseru Mseru na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Muhimbili, Prof Joseph Kuzilwa,  walivyokuwa wakijitahidi kuongea na kuonyesha uzuri kwa serikali. Mfano prof Mseru yeye anasema hali ya vifaa na vitendea kazi pale MOI ni nzuri sana... wakati Dr. Marina Njelekela anasema vifaa pale Muhimbili vipo vingi sana tu tatizo ni idadi ya wagonjwa kuwa kubwa...hata hivyo anataja hata CT Scan, ilhali inaeleweka kwamba iliharibika na haikutengenezwa kwa zaidi ya miezi sita!!! Usaliti wa kisomi huu.
Prof Kuzilwa

Kubwa zaidi ni msisitizo aliotoa CEO wa Muhimbili dr Marina Njelekela juu ya madaktari kuongozwa na MORAL OBLIGATIONS. Alilisisitiza sana hili kuwa ndiyo mwarobaini wa kutatua migogoro miongoni mwa wanataaluma na wataalam wa afya. Moral obligations ama maadili ya kazi ya udaktari inahusiana na ukweli kwamba taaluma na utaalamu huu unahusisha kuokoa maisha ya binadamu wenzao (pale Mungu anaporuhusu hilo litimie).
Nakubaliana na mtaalam na kiongozi huyu muhimu wa sekta ya afya. Hata hivyo, nadhani ilikuwa sahihi zaidi pia kugeuza kibao hicho cha obligations kwa upande wa serikali. 

Haitoshi kuendelea kuwakandamiza wataalam wetu hawa wachache wa tiba kisa, vile tu maadili ya kazi yao haiwaruhusu kugoma kama njia ya kuepusha migogoro. Serikali isiyokuwa na maadili, isyojali moral obligations, inaziba masikio na kuziba channels zote za kutatua migogoro na kutanzua kero za waganga kwa sababu wanajua madaktari hawataweza kugoma. 

Mtangazaji Shaaban Kisu (Kulia)
Pia nadhani ni wakati muafaka kuacha kuwalaumu madaktari eti si wavumilivu. Na hapa ndipo kaka Shaaban Kissu ambambo alinikosha kwa kuuliza, hivi madai ya madaktari ni mapya?  Wasomi hawa wakabaki wanajibu kwa kujiumauma.

Ufike wakati kauli ya moral authority isisitizwe kwa kila mmoja lakini serikali ndiyo iwe ya mfano. Iache usanii huku ikitegemea watanzania wengine wataendelea kuwa waadilifu. Kilichotokea kiwe fundisho muhimu sana kwa kila mtanzania lakini zaidi kwa serikali na vibaraka wake katika sekta ya afya.

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP