Pekua/search

Monday, October 22, 2012

Mfumo DUME hauna UUME wala NDEVU



Mfumo DUME hauna UUME wala NDEVU

Mambo yalikuwa hivi mkutanoni. Mama Sofia Simba kwambali kama anatamani kuinuka vile. Picha toka ukuta wa fb wa gazeti mwananchi.

Ukiiangalia picha hii na ukifuatilia kwa karibu zogo lililozuka kwenye mkutano mkuu wa uchaguzi wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) huko Dodoma,unapata picha kwamba MFUMO DUME umetawala maisha yetu Watanzania na ni hatari zaidi maana kuuondoa hakuishii tu kuongeza idadi kubwa ya wanawake kwenye nafasi za maamuzi.

Ningetarajia kuuona MFUMO USAWA ama basi MFUMO JIKE katika uchaguzi ule. Lakini kilichotawala pale ni mfumo dume uliopindukia ule unaofanywa na wanaume. Kitendo cha kutaka baadhi ya watu tena wenye dhamani WASIHOJIWE na WASITOE MAELEZO kwa wajumbe, kitendo cha kutaka wajumbe WANYAMAE Ndiyo hasa MFUMO DUME wenye. Mfumo dume kwa sifa zake na rangi yake halisi sit u kule kupendelea wanaume katika kufanya maamuz na katika kupata na kutumia fursa, bali ni mfumo NYAMAZISHI, HODHI usiotaka HOJA bali AMRI.

Mjumbe kamuuliza mgombea amefanya nini ama juhudi gani kukiimarisha chama chao? Hilo linaletaje zogo? Badala ya kujibu hoja na kuwafahamisha wajumbe mgombea anarusha vijembe juu ya uchanga wa muuliza swali...’mgni huyu...hajui tulichofanya...JAMANI SI NDIO MAANA ANAULIZA? Kama kawaida yao wapambe wamekuwa mstari wa mbele kutaka kumnyofoa macho mjumbe aliye hoji..huu ndiyo mfumo dume hasa. Mfumo usiovumilia fikra tofauti na mawazo mbadala.

Mlioko kwenye harakati dhidi ya mfumo dume hamna budi kuutambua mfumo huu vizuri..hauna ndevu wala uume..ni mfumo unaowaumiza wanawake kwa wanaume sawia..hata baadhi ya wanawake wanautumia mfumo huu kuwaumiza na kuwakandamiza wanawake wengine.

4 comments:

Anonymous October 22, 2012 at 1:03 AM  

Ni kwel kabisa, Tunataka kuona mfumo unaotoa haki na fursa sawa kwa watu wote, lengo si kuondoa mfumo dume na kuweka mfumo jike, Lengo liwe kuweka mfumo unaotoa usawa kwa watu wote. Ndio maana wanawake hawawezi kucompete kwa sabb wao kwa wao hawapendi kuinuana na kushirikiana na kupaza sauti zao kwa pamoja

Adam October 22, 2012 at 2:07 AM  

Hakika. Mfumo sawia ama mfumo haki ndiyo unaohitajika, ila ndiyo tuko mbali sana. maana makamanda wenyewe ndiyo hao kina nanilii wanavuruga mambo.
Hawataki mawazo tofauti..hawana subira

Saidi R. Fundikira October 23, 2012 at 12:51 AM  

Swadakta mlionitangulia kutoa maoni.. Mimi napendekeza tulichambue tukio hili, na dhana yote ya jinsia kwa kina zaidi. Tujiulize je dhana hii yote ya Jinsia haukuchangia tu, kama si kuanzisha na ku_instutionalize ubaguzi katika jamii? Je haya yote ya madkatari(wanawake), Chama (wanawake) nk hayatufikisha katika TAnzania (Wanawake), Je Mwl JK Nyerere alipotuasa tuache ubaguzi akifikiria mambo ya hivi pia? Je, divide and rule inafanya kazi hapa? Mengi tujiluize wabongo wenzangu, binaadamu wenzangu!

Adam October 23, 2012 at 1:06 AM  

Saidi, shukrani kwa mchango wako mwanana kwa maana unafikirisha. Nadhani kuwepo ...wanawake, kwa maoni yangu sio msingi wa ubaguzi. ndiyo uhalisia wenyewe, kuna wanaume na wanawake katika taifa hili na wanauhitaji unaotofautiana katika mazingira na nyakati fulani fulani. Na ndiyo maana wimbo wetu wa taifa umekuwa miongoni mwa nyimbo zilizo gender sensite zzaidi duniani...Wake kwa waume na watoto...jamii sio homogenous.

Kamba ubaguzi ni state of mind, ndiyo msingi wa kuandika post hii hata kwa kutumia maneno yasiomazuri sana kama 'uume'. Nafsi ikishachafulika, basi utambagua hata mwanao wa kumzaa. ndicho kinachotokea, kuna wa kundi hili na wa kundi lile, basi wanajisahau kabisa kina mama hawa kuwa wote ni wana wake na ni wa tanzania.
Tuendelee kuchangia

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP