Pekua/search

Thursday, January 17, 2013

Pongezi Salma Kikwete kuhutubia kwa Kiingereza siku hizi.


Pongezi Salma Kikwete kuhutubia kwa Kiingereza siku hizi.
Mama Salma Kikwete

Hongera mama Salma Kikwete kwa hatua uliyopiga. Uko juu mamaaetu!!! Kumbe unaweza kuhutubia kwa lugha ya KIINGEREZA siku hizi!!! Ila ndiyo umenivunja moyo ile mbayaaaaaaaaaa….

Nimebahatika kwa kushuhudia mwenyewe si kama nilivyokuwa naambiwa, kuwa mama yetu mama kiongozi, na kiongozi wa shirika la WANAWAKE NA MAENDELEO, Salma, nahutubia hadhara za kimataifa siku hizi kwa Kimombo. Nimemshuhudia mimi mwmenyewe kwenye TV (analojia) akihutubia kwa Kiingereza kizuri sana leo huko mjini Arusha.

Lakini Kwanini hiyo imenivunja moyo na kuisononesha nafsi…soma hapa:
Baada ya Rais Jakaya Kikwete kuingia madarakani mwishoni kabisa mwa mwaka 2005, mama Salma alikuwa akihutubia kwa lugha ya adhimu ya Kiswahili kwenye hadhara zote iwe za kitaifa na kimataifa. Alinikuna kweli kweli. Akanifanya niondoke mafichoni, nirejee kwenye fani, nikaishika kalamu makala gazetini nikaandika (http://www.upolesana.blogspot.com/2009/09/kujifunza-kwa-salma-kikwete-kuhusu.html) Sikusema jingine lolote bali kumwagia sifa mke wa rais wetu, mama yetu kwa kukienzi Kiswahili. Nikijua kwamba kwa hadhi yake ya ualimu, alikuwa akikijua kiingereza cha kutosha, lakini alichagua uanaharakati wa kukuza Kiswahili. Hakika nilimwelezea kuwa ni mama kiongozi wa mfano..

Niliona mama Salma akijipambanua vizuri sana katika matumizi ya Kiswahili. Nilifurahia hata kuanzisha asasi ya WAMA, yaani Wanawake na Maendeleo ikiwa katika jina la Kiswahili pengine tofauti na menginyo tuliyoyazoea, kama vile ‘Iko potyuniti fo alu ’. Nikamwona yu mama wa mfano kweli kweli ambaye hata alimpa changamoto mumewe, Rais wetu katika kuiendeleza lulu hii, ambayo si tu ni fahari kwetu bali ni fursa ya utajirisho.

Ziko faida kubwa kwa viongozi wetu KUTUMIA Kiswahili mbali ya fahari, iko faida kwamba kuna watanzania wanapata kazi kwa mfano, kufasiri na kukarimani. Kiswahili kinaongeza mvuto na ladha yake kunoga zaidi. Nikiri kwamba sifahamu, ni mjinga mimi mathalani, sijui inakuwa vipi viongozi kama Obama wakienda Korea, Japani koote huko, hivi viongozi wan chi hizo hulazimika kuongea Kiingereza, ambayo wengi tunaipamba kuwa lugha ya dunia na ya lazima? Aaaagh mama Salma….!!!!!!!!Naam, siku hazigandi…Lakini NAKUPONGEZA TU kwa kuwa mjanja zaidi kuweza kuumwaga ung’eng’e, ni maendeleo pia.


0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP