Pekua/search

Saturday, April 20, 2013

Naunga mkono 'ukorofi' wa wabunge 'wakorofi' Bungeni


Naunga mkono 'ukorofi' wa wabunge 'wakorofi' Bungeni


Nachukua fursa hii kuwapongeza kwa dhati kabisa wabunge wa Upinzani Bungeni wanaojitoa kimasomaso kukabiliana na kanuni na taratibu kandamizi kwa ustawi wa taifa letu. Msingi wa pongezi hizi uko katika usemi unaodai “Good People Disobey Bad Laws” yaani Watu wema Hawatii Sheria mbovu.  Shime wabunge wa upinzani, endeleeni kutuondoa kwenye ka ‘comfort zone’ ketu tulimodumu kwa miaka nenda rudi na kujikuta leo hii tumefika hapa taifa limegota na kusuasua tu kwa kufanya mambo kimazoea.


Heri hili bunge linaloonekana la vurugu lakini mawaziri wanalazimika kufikiria mara mbili mbili wanapojiandaa kuepeleka hoja zao; kuliko bunge la ‘kishemiwa’ na ‘staha’  ambamo serikali inajiachia itakavyo kwa kujua itaungwa mkono mia kwa mia asilimia!


Bora mkaonekana wakorofi kwa kuuliza mwongozo mara kwa mara na kupigania haki na masuala muhimu yanayofunikwafunikwa kama kuumizwa kwa Dkt Ulimboka na kuuawa kwa Mwangosi; kuliko kuonekana ‘wastaarabu’ kwa kutukana mitusi mizito kama FUCK YOU!


Heri mkaonekana na kuitwa majina yoyote mabaya yaliyopo duniani (comedians, wataka sifa, msiojitambua nk nk) mkizikinza kanuni na taratibu zinazodidimiza nchi kuliko mkaonekana wastaarabu mnaounga mkono hoja mbofumbofu!!!


0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP