Pekua/search

Thursday, June 28, 2012

SERIKALI ITATUE MATATIZO SEKTA YA AFYA IACHE VITISHO

  • Iongoze bajeti ya afya
  • Ibane matumizi kwa kuacha kuongeza wilaya na mikoa na ivunje baadhi ya balozi zake nk.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya madaktari Dkt Steven Ulimboka akiwa amejeruhiwa vibaya


Kuna taarifa kwamba tayari serikali imeanza kuwafukuza kazi madaktari wanapigania kuboreshwa kwa huduma za afya nchini ikiwa ni pamoja na maslahi yao. Mbali ya kauli za vitisho zilizotolewa na viongozi wakuu wa serikali kuhusu migomo hususan wa madaktari, serikali imeshindwa kusimamia wajibu wake.

Yangu ni machache tu kuwa;
 
  • Wajibu wa serikali ni kukusanya raslimali za nchi ikiwemo kodi na ushuru mbali mbali na kuzitumia raslimali hizo kutoa huduma zote za msingi kwa raia wan chi hiyo. Huduma ya afya ni msingi wa misingi yote.
  • Wajibu wa wananchi ni kutoa hizo kodi, na kuzilinda na kuzitumia kwa uendelevu mali asili zilizopo kwenye maeneo yao.
  • Kwa wataalam, kama madaktari walisomeshwa na serikali, sio kwa hisani bali katika kuwajibika kutimiza wajibu wake(serikali) wanawajibika KUTIMIZA WAJIBU wao na KUPIGANIA KUBORESHWA KWA MAZINGIRA YANAYOHITAJIKA ILI KUTIMIZA WAJIBU WAO.

Serikali ibane matumizi yake na kuachana nay ale yasiyo ya lazima kama kuendelea kuongeza mikoa na wilaya (ukoloni) badala ya halmashauri za wilaya, miji na manispaa (tawala/serikali za wananchi), itimize wajibu wake kwa kutekeleza kile kilichofanya madaktari wakubali kurudi kazini pale awali. Bora serikali ikavunja hata balozi zake nyingine ambazo hazina tija kubwa katika kuiendesha nchi hii (tubaki na zile za kimkakati tu). Serikali itenge bajeti ya kutosha kwa huduma za afya ili kuung’oa mzizi wa fitna. Hakuna njia ya mkato.
Kuwafukuza madaktari ni kuzidi kutoa hukumu ya kifo kwa watanzania tulio wengi. Je kama haina fedha za kutosha kutimiza madai ya madaktari ya kuboresha huduma za afya, itawezaje kutafuta madaktari mbadala ambao wengi ni ghali? SERIKALI IKOME KUTOA VITISHO. WANAWEZA KUMUUA DKT MMOJA, LAKINI HAITAWEZA KUDHIBITI GHADHABU YA WANANCHI INAYOZIDI KUONGEZEKA.

Kwa kuhitimisha niungane na kauli ya Mbunge wangu wa Ubungo John Mnyika,
“Sababu ya hali tete ya nchi na maisha ya wananchi kwenye sekta ya afya ni udhaifu wa serikali na uzembe wa bunge. Rais Jakaya Kikwete ajitokeze alitangazie taifa kuunda tume huru ya kuchunguza kutaka kuuwawa kwa Dk. Ulimboka Steven na kutoa ahadi ya kuongeza fedha katika bajeti ya wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2012/2013 ili kushughulikia chanzo cha mgogoro. Spika Anna Makinda aruhusu bunge litumie mamlaka yake ya kuisimamia serikali kusuluhisha.”

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP