Pekua/search

Saturday, August 25, 2012

Dar na miji mingine ingekuwa Yatima leo hii- SENSA NJEMA


Utaratibu wa Sensa usingebadilika-  Dar na miji mingine ingekuwa Yatima leo hii

“Siku zile amri  ilitoka kwa Kaisari Augusto ya kwamba IANDIKWE ORODHA YA MAJINA YA WATU WOTE (SENSA) wa ulimwengu (nchini mwake). Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyoandikwa hapo Kirenio alipokuwa liwali wa Shamu. Watu wakaenda kuandikwa, kila mtu  mjini kwao. Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa ukoo na jamaa ya Daudi, ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa naye ana mimba, ikawa katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia, akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori la kulia ng’ombe, kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni. “ Luka Mtakatifu – 2: 1- 7.

Haya wandugu HESABIWENI. Enzi za wenzetu ingebidi Dar es Salaam kwa mfano ibaki na watu wachache tu.
Jikumbushe kuhusu sense nchini:
Sensa ya kwanza Tanzania ilifanyika mwaka 1910. Sensa nne za Mwisho zilifanyika baada ya Uhuru, katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002.
Kulingana na sensa ya mwisho iliyofanyika mwezi Agosti 2002, idadi ya watu nchini Tanzania ilikuwa 34,443,603.
Waziri Mkuu Pinda alipozindua uhamasishaji wa Sensa ya Watu na Makazi 2012

Matokeo ya Sensa ya Watu 1967-2002 na Makadirio kati ya mwaka 2003-2025 Mwaka Idadi Mwaka Idadi
1967 12,313,469
1978 17,512,610
1988 23,095,885
2002 34,443,603
2003 34,859,582
2004 35,944,015
2006 38,250,927
2009 41,915,880
2010 43,187,823
2012 45,798,475
2015 49,861,768
2020 57,102,896
2005 37,083,346
2025 65,337,918
Rais kikwete alipohutubia taifa kuhamasisha ushiriki katika Sensa jana. Picha kutoka Twita ya Haki Ngowi.

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP