Pekua/search

Friday, April 5, 2013

CCM Kitaachwa kiwakumbatie Mafisadi mpaka lini?



CCM Kitaachwa kiwakumbatie Mafisadi mpaka lini?
 
Nape Nnauye. Krediti: Gazeti Mwananchi
Wengi wameshitushwa na habari iliyotolewa na gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi tarehe 4 Aprili mwaka huu kuwa kamanda wa upambanaji dhidi ya ufisadi Dkt Harrison Mwakyembe naye ni fisadi (http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=47479 ). Bahati nzuri chama cha mapinduzi CCM kupitia katibu wake mwenezi Nape Nnaye  kimejibu tuhuma hizo na kusisitiza kwamba zabuni hata haijapewa kampuni ya chama hicho bado.   Lipi ni sahihi tunaendelea kuchakata kwenye mbongo zetu na waandishi wa habari uchunguzi watatujuza inshallah.

Katika taarifa ya Nnauye aliyoitoa kwa vyombo vya habari anaeleza yafuatayo,
Lakini tunazo taarifa kuwa uongo huu wamelishwa na baadhi ya mafisadi waliotakakutumia eneo hili la CCM kujaribu kukaa katikati ya mwekezaji yeyote atakayejitokeza na Jitegemee kwa lengo la kujinufaisha wao binafsi. Na huu ni mwendelezo waChadema kutumiwa na mafisadi katika kutimiza mambo yao.”...anahitimisha taarifa hiyo kwa kusema, “Tunawataka wasikatishwe (wizara ya uchukuzi chini ya Mwakyembe)  tamaa na mafisadi wachache,wachape kazi kwa uzalendo huohuo waliouonesha.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo kwa mara nyingine CCM kinaeleza waziwazi kuwa kinawafahamu mafisadi na kwamba kinajua kuwa mafisadi wamekuwa wakikitumia CHADEMA. Hawa mafisadi ni kina nani? Wako chama gani? Yawezekana wakawa chama chochote ama hawana chama kabisa, lakini je  CCM ambacho ni chama tawala pamoja na serikali yake kinafaidika vipi kwa kuwatazama tu hawa mafisadi? Kitaendelea kuwafuga hata lini? Najiuliza tu.

Wakati umefika wa moja ya mambo haya kufanyika;
(i)            CCM kuiagiza serikali yake kuwashughulikia mafisadi au
Watanzania kukiwajibisha chama hiki kwa kukumbatia mafisadi

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP