Pekua/search

Tuesday, May 7, 2013

NANI AFANYE NINI?

Bibi yangu miaka ishirini iliyopita aliniambia maneno ambayo sijapata kuyasahau. Nilikuwa nimefadhaika sana ndipo katika mfadhaiko huo nikapata kutamka kitu ambacho kiliamsha hekima ya Marehemu bibi. Aliniambia 'ukiwa na furaha mwanangu (alizoea kuniita mwanae) usiahidi kitu, ukiwa na huzuni usitamke neno lolote na ukiwa na njaa usiahidi kitu'. Nimejitahidi sana kuishi katika hekima hii ingawa kuna muda huwa napotea maana ndio ubinadamu.
Nimeikumbuka hekima hii muda huu baada ya kusikia maana ilitangazwa kwenye redio na kusoma kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusu mlipuko wa bomu (ingawa kuna baadhi ya TV zinaripoti kuwa kitu kinachohisiwa kuwa bomu! iwe vyovyote) uliotokea Arusha! Ni muendelezo tu wa yale yaliyotokea siku za nyuma, zilianza kama cheche, sasa zinakuwa si cheche tena! Nilitaraji mtu mmoja angezizima cheche hizi kwani moto hufa kwa kukosa kuni, lakini haijawa hivyo, bali nguvu nyingi zimeelekezwa kuzikataa cheche ambazo zinaongezeka.
Ndipo nikajiuliza niseme nini wakati huu wa fadhaa maana nachelea sana kumlaumu mtu, sasa nifanye nini? Je nikae kimya? Mpaka lini? ndipo nikasema nami niseme japo humu tu. Kwamba nitasikika sijui maana mimi ni mtu mdogo sana, tena sifahamiki kwa yoyote, laiti ningekuwepo mjengoni ningepaza sauti na kutunisha msuri pengine nikiunga mkono hoja,,,maana pasipo hivyo nitatukanwa nami sipendi matusi,,after all its about how much i make in the evening after a single sitting,,hadi raha kukaa tu hela,,,laiti wote tungekaa na kupata hela ingekuwa njema sana,,mmmh nisitoke kwenye hoja yangu ya msingi may be just may be siku moja nitasema umuhimu wa kukaa na kupata pesa,,maana iliandikwa zamani sana ,,KAENI NDANI YANGU,,,,,
Najiuliza nani afanye nini ndio swali langu. Ni kweli tumetikiswa na bomu, ni kweli Padri aliuwawa Zanzibar, je ni kweli vyombo vyetu TUKUKA havijaweza chunguza na kusokotoa nani kahusika? Je tumeshindwa kuwabaini hawa wabaya wanaotugawa sasa? Kuna udhaifu gani huo kupelekea kuwaomba FBI waje kwetu kuchunguza? Je wanachunguza hayo tu au na udhaifu wetu mwingine? Mbona tumeweza kwenda DRC na JESHI LETU TUKUKA? Tumeanguka wapi mpaka kuwaomba hawa FBI? Je yalipotokea mabomu kwenye MBIO za marathoni walituomba? ooh sorry they are better than us,,Je wataishia tu kuchungua bomu? Twahitaji sana kujua nani afanye nini wakati gani,,je si mwenye msiba aliaye sana kuliko waliokuja kuomboleza? Haya maadamu hatujiamini tena nachelea kusema hawa jamaa hawatatuacha mpaka wametuchunga oooh wametuchunguza na kutujua sana zaidi ya tujijuavyo,,mwisho wa siku tutawaomba wawe sungusungu wetu na ndipo tutawatumikia,,,,

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP