Pekua/search

Thursday, November 14, 2013

Mauaji ya Dkt. Mvungi- Jambazi Sugu hili hapa



 Mauaji ya Dkt. Sengondo Mvungi- Jambazi Sugu  hili hapa

Suleiman Kova, Kamanda Kanda Maalum Dar es Salaam
 Jambazi sugu hili hapa, mwaliona?
Limeshiriki kumuua dakta wetu Sengondo Mvungi, nani atapona?
Huenda na wengine kama Jwani, nani atakana?
Na kujeruhi wengine kama Dkt. Ulimboka, inawezekana!
Ni jambazi sugu hili, licheki lilivyo pozi, si mwaliona?
Ni jambazi sugu hili lilipohojiwa limekiri, bila kujibana!
Na limekiri haraka kweli kweli,pasikubishana!
Limejitolea kutuonesha na bastola ya dakta Mvungi, hakuna kusigana!
Ndiyo, ni lijambazi sugu limekamatwa likiangalia RUNINGA!
Jinale Ngosha, John Mayunga!

Jamani lijembawazi hili si mmeliona?
Mmelitazama vizuri lakini?
Hilo hapo msijeleta visingizio,
mkadhani ni njama. Ni ujambazi!

Jamani hizi sio ngojera za kuburudisha tu, sawa?
Bali ni TAMthilia (sema CHUNGU) iliyosukwa mahsusi, haina dawa!
Msijesema mlizisikia kwa ulimboka na Yule Mulundi, Mkenya, si ilikuwa powa?
Msijesema ni zile zile, msijifanye mmezizoea, mtabishiwa!
Hili ni lijambazi sugu, si  lilifungwa?,
Limetoka jela, au mwadhani  mahsusi limetolewa?
Ndiyo, hata kama bado halijatoka, si vibaka walitumwa?.
Vibaka kwa kawaida hawahitaji mali ama fedha, Mwaelewa?
Hutaka laptop na nyaraka, si ni vibaraka wenye viraka?

Shenzi zao vibaka wanaopenda kudaka laptop!
Pumbavu zao vibaka hawa wanaohitaji nyaraka nyeti

Oh no! na jambazi sugu lilikuwepo.
Li John Mayunga, Ngosha si la depo!
Tena na baruti zilikuwepo
Hata haya yatapita kama upepo.
Viva Kamanda Kova! Kazi nzuri.
Endelea mpaka mwisho.
Buriani Msomi Mweledi Sengondo Mvungi.
Kwaherini.
Dkt.Sengondo Mvungi, Pumzika kwa Amani

1 comments:

Unknown December 1, 2013 at 4:59 AM  

hilo jamaa ni kiboko ya maboko.

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP