Pekua/search

Thursday, May 1, 2014

Tanzania: Yuko Wapi Kiongozi wa Ukweli mtu wa watu?



Benjamini Mkapa- Uwazi na Ukweli?

Yuko Wapi?

Yuko wapi Kiongozi jabari na mweledi?

Yu wapi kiongozi Mahiri? Yuko wapi shupavu?

Yu wapi Kiongozi mwenye nia thabiti ya kuchochea maendeleo ya taifa hili?
Yuko wapi kiongozi wa ukweli

Yuko wapi aliye madhubuti na hodari kiuongozi akemee Zanzibar kujitungia katiba yenye kuchepusha muungano? Yuko wapi?

Yuko wapi kiongozi kati ya hawa wa kwetu katika chama tawala na kwenye vyama vya ushindani, mwenye kuupenda muungano? Yu wapi?

Nani kati yao hawa wetu viongozi mwenye kuenzi fikra na matendo ya Mwalimu Nyerere kwa kumaanisha? Yuko wapi?

Yuko wapi kiongozi anayeamini kuwa siasa si mchezo mchafu wa ghiriba, hila na ‘usanii’? mmemwona wapi?

Jakaya Kikwete- za kuambiwa ongeza za??
Yu wapi kiongozi hapa nchini anayeamini kabisa kabisa kuwa mamlaka ya nchi yanatokana na watu wana wananchi? Yuko wapi?

Yuko wapi kiongozi anayeupenda Muungano kwa dhati ya moyo wake? Yuko wapi? Tanzania inamtaka na atamke sasa kwamba Muungano wa serikali mbili ziiiiiiiiiii!!!!

Na aseme sasa kwamba muungano wa serikali tatu ziiiiiiii bali twende kwa serikali moja muungano kamili?

Tuamini YUPO. Tuafiki WAPO.
Lakini wako wapi? Kwanini wanajificha? Kwanini midomo yao inakuwa mizito na matendo kwao ni muhali kufanyika?

Yuko Wapi Kiongozi wa Ukweli mtu wa watu? Yuko wapi kiongozi mwenye dhamira ya dhati?
Alhaji Ali Hassan Mwinyi- Ruksaaa- na li kul-li ajalin kitaab.

0 comments:

SUBSCRIBE- Andika email yako hapa utumiwe habari mpya

Enter your email address:

Delivered by FeedBurner

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.com 2008 modified by Subi nukta77

Go Back to TOP